BUKOBA SPORTS

Wednesday, November 28, 2012

ENGLISH PREMIER LEAGUE: SUNDERLAND 0 vs QPR 0, ASTON VILLA 1 vs READING 0. HARRY REDKNAPP AKARIBISHWA QPR KWA DROO NA SUNDERLAND!!, WAO ASTON VILLA WAICHAPA READING GOLI 1-0

Harry Redknapp akiangalia vijana wake bila matumaini ya kupata goli

Ligi kuu England (EPL) imeendelea leo katikati ya wiki na leo hii kumekuwa na mechi mbili tu Sunderland wakimkaribisha QPR ambao wapo mkiani. Aston Villa wao wamewakaribisha Reading kumbuka timu hizi mbili zinasua sua mpaka sasa zipo nyuma.

Harry Redknapp (kocha mpya QPR) leo ameanza kibarua kigumu cha kuinasua na kuinusuru QPR kutoka mkiani mwa Ligi Kuu England kwa kucheza Mechi ya ugenini na Sunderland huku mwenyewe akiwa tayari amekiri kuwa hii ndiyo changamoto kubwa kabisa katika maisha yake yote ya Ukocha na vile vile kuwaambia Wachezaji wake kuwa ni fedheha kwa QPR kuwa mkiani na ni aibu kwa Wachezaji.
Harry Redknapp akitoa maelekezo kwa timu yake


Gabriel Agbonlahor (kushoto) wa Aston Villa akikabwa vilivyo na Shaun Cummings
Robert Green akijitupa kwa Steven
Early end: Villa defender Enda Stevens (centre) had to be replaced after picking up an injuryEnda Stevens (katikati) alibadilishwa baada ya kuumia hapa

RATIBA/ MATOKEO
Jumanne Novemba 27
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Sunderland 0 vs QPR 0

Aston Villa 1 vs Reading 0
[SAA 5 Usiku]


Wakati Redknapp anaanza kibarua kipya katika Klabu yake ya 5 ya Ligi Kuu England, nyingine zikiwa ni Portsmouth, Southampton, West Ham na Tottenham, hii ikiwa ni rekodi, Meneja wa Sunderland, Martin O'Neill, nae ana wakati mgumu kwani Sunderland inasuasua na imeshinda Mechi mbili tu za Ligi Msimu huu, moja tu ikiwa Uwanja wa nyumbani tangu Mwezi Machi.

Huku akikabiliwa na Mechi dhidi ya Manchester United na Chelsea mwanzoni mwa Desemba, bila shaka Martin O'Neill ataona nafasi ya wazi ya ushindi ni Mechi hii na QPR.

Rose na Jamie Mackie wakigombania mpira leo hii usiku
Kipa Simon Mignolet akijionea mambo yao kuwa magumu sana

VIKOSI
Sunderland: Mignolet, Bardsley, Kilgallon, Cuellar, Rose, Cattermole (Colback 6), Larsson, Gardner (Saha 78), Johnson (McClean 70), Sessegnon, Fletcher,
Subs not used: Westwood, Bramble, Vaughan, Campbell
Booked: Cuellar


QPR: Julio Cesar (Green 46), Traore, Hill, Nelsen, Bosingwa, Diakite (Park Ji-sung 65), Taarabt (Wright-Phillips 77), Granero, M'bia, Cisse, Mackie
Subs not used: Ferdinand, Fabio, Derry, Hoilett
Booked: Diakite, Hill, Mackie
Referee: Andre Marriner
Attendance: 36,513



RATIBA MECHI ZIJAZO
Jumatano Novemba 28
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v Fulham
Everton v Arsenal
Southampton v Norwich
Stoke v Newcastle
Swansea v West Brom
Tottenham v Liverpool
[SAA 5 Usiku]
Wigan v Man City
Man United v West Ham
 

Jumamosi 1 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Ham v Chelsea
[SAA 12 Jioni]
Arsenal v Swansea
Fulham v Tottenham
Liverpool v Southampton
Man City v Everton
QPR v Aston Villa
West Brom v Stoke
[SAA 2 Dak 30 Usiku]
Reading v Man Utd
 

Jumapili Desemba 2
[SAA 1 Usiku]
Norwich v Sunderland
 

Jumatatu Desemba 3
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Wigan

No comments:

Post a Comment