
RATIBA:
[Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku Bongo Taimu]
Jumanne Novemba 6
FC Dynamo Kyiv v FC Porto
Paris SaintvGermain FC v GNK Dinamo
FC Schalke 04 v Arsenal FC
Olympiacos FC v Montpellier Hérault SC
RSC Anderlecht v FC Zenit St. Petersburg
AC Milan v Málaga CF
Manchester City FC v AFC Ajax
KUNDI B
FC Schalke 04 v Arsenal FC
MSIMAMO
[Kila Timu imecheza Mechi 3]
1 Schalke Pointi 7
2 Arsenal 6
3 Olympiacos 3
4 Montpellier 1
Wiki mbili zilizopita, Schalke
waliinyuka Arsenal 2-0 Uwanjani Emirates kwa Mabao ya Kipindi cha Pili
ya Wachezaji wa Holland, Klaas-Jan Huntelaar na Ibrahim Afellay.
Lakini zote, Schalke na Arsenal,
Jumapili zilifungwa katika Ligi zao kwa Schalke kupigwa na Timu goigoi
Hoffenheim kwenye Bundesliga na Arsenal kuchapwa 2-1 na Man United
kwenye Ligi Kuu England.
Nahodha wa Shalke, Benedikt Hoewedes,
amesema Kikosi chao kitakuwa na nguvu wakicheza Uwanja wa nyumbani na
amehoji: “Tulishinda London, kwa nini tusishinde nyumbani
Veltins-Arena?"
Tangu wafungwe nyumbani na Schalke,
Arsenal wamekuwa wakisuasua na kupata ushindi mwembamba wa Bao 1-0 dhidi
ya Timu ya mkiani QPR, kisha kuibuka toka kichapo cha 4-0 na kuitwanga
Reading 7-5 katika CAPITAL ONE CUP na kuja kufungwa 2-1 Old Trafford na
Man United kikiwa ni kipigo cha 3 katika Mechi zao 5 za mwisho.
Kwenye Mechi hii na Schalke Meneja wa
Arsenal, Arsene Wenger, atamkosa Gervinho ambae atakuwa nje kwa Wiki 3
na pia majeruhi wengine ambao wamepona lakini hawajawa fiti ni Kieran
Gibbs, Kipa Wojciech Szczesny, Abou Diaby na Tomas Rosicky.
KUNDI D
Manchester City FC v AFC Ajax
MSIMAMO
[Kila Timu imecheza Mechi 3]
1 Borussia Dortmund Pointi 7
2 Real Madrid 6
3 Ajax 3
4 Manchester City 1
Jumanne Usiku, Man City watakuwa
nyumbani kurudiana na Ajax ambayo iliitwanga City 3-1 katika Mechi
iliyopita Wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo, Mancini amekiri wanahitaji
miujiza ili kufuzu kutoka Kundi ambalo lilibatizwa ‘Kundi la Kifo’ na
amesema: “Sidhani kama tuko tayari kutwaa Ubingwa wa Ulaya. Sisi ni Timu
nzuri lakini hatuko tayari kama Timu nyingine. Pengine Chelsea walikuwa
Timu nzuri Ulaya kwa Miaka 10 na wamechukua Ubingwa baada ya Miaka 10,
pengine hawakustahili!”
RATIBA:KESHO
[Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku Bongo Taimu]
Jumatano Novemba 7
Juventus v FC Nordsjælland
Chelsea FC v FC Shakhtar Donetsk
Valencia CF v FC BATE Borisov
FC Bayern München v LOSC Lille
SL Benfica v FC Spartak Moskva
Celtic FC v FC Barcelona
CFR 1907 Cluj v Galatasaray A.S.
SC Braga v Manchester United FC
No comments:
Post a Comment