
Habari hizi zimetolewa na Bodi ya Leicester City na zimekuja Siku 1 tu baada ya Klabu hiyo kufungwa 2-1 huko Spain na Sevilla katika Mechi yao ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Ranieri, mwenye Miaka 65, aliiongoza Leicester, kwa mshangao wa wengi, kutwaa Ubingwa wa England Msimu uliopita wakiwa mbele kwa Pointi 10 lakini Msimu huu mambo yako mrama na wako hatarini kuporomoka Daraja.
Leicester wamepoteza Mechi zao 5 za Ligi zilizopita na ndio Klabu pekee katika Madaraja yote Manne ya England ambayo haijafunga hata Bao 1 la Ligi Mwaka huu 2017.
Mechi ijayo kwa Leicester ni kwao King Power Stadium Jumatatu ijayo dhidi ya Liverpool.
No comments:
Post a Comment