8 Agosti 2015: Mourinho amshutumu Carneiro kwa kuwa "mjinga"
22 Septemba: Carneiro anaachana na Chelsea
30 Septemba: Mourinho asafishwa na FA kumshutumu Carneiro
30 Septemba: Uamuzi wa FA kuhusu Mourinho wapingwa na Makundi
1 October: Bosi wa FA Dyke amponda Mourinho
Sakata la Dokta Eva Carneiro na Mourinho liliibuka kwenye Mechi ya Agosti 8 ya Ligi Kuu England waliyotoka 2-2 na Swansea City Uwanjani Stamford Bridge.
Katika Mechi hiyo,Dokta Carneiro na Tabibu wa Viungo Jon Fearn waliingia Uwanjani kumtibu Eden Hazard kwenye Dakika za Majeruhi wakati Chelsea ipo 2-2 na Swansea City huku wakiwa Mtu 10 baada ya mapema Kipa wao Thibaut Courtois kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Kitendo hicho kilimkera Mourinho kwani Mchezaji akihudumiwa na Madokta basi huwajibika kutoka nje ya Uwanja na husubiri amri ya Refa kuingia tena huku Gemu ikiendelea na hilo liliiacha Chelsea iwe Mtu 9 kwa Dakika kadhaa.
Mourinho alimponda Dokta huyo na kumsema hajui mchezo unakwendaje.
No comments:
Post a Comment