Tuesday, March 5, 2024

Draw Date confirmed for TotalEnergies CAF Champions League and Confederation Cup Knockout Stages


The Quarter-Final draw for the 2023/24 TotalEnergies CAF Champions League and TotalEnergies CAF Confederation Cup will be conducted on Tuesday, 12 March 2024.

The draw will be conducted in Cairo, Egypt starting with CAF Confederation Cup at 14h00 Cairo time (12h00 GMT) and CAF Champions League at 15h00 Cairo time (13h00 GMT).

The teams that will participate in the Quarter-Finals of the TotalEnergies CAF Champions League and TotalEnergies CAF Confederation Cup are known following the conclusion of the group stage over the weekend.

TotalEnergies CAF Champions League Quarter-Finals Qualified teams:

Al Ahly (Egypt), ASEC Mimosas (Cote d’Ivoire), Mamelodi Sundowns (South Africa), Atletico Petroleos (Angola), TP Mazembe (DR Congo), Simba SC (Tanzania), Esperance Sportive de Tunis (Tunisia), Young Africans (Tanzania).

TotalEnergies CAF Confederation Cup Quarter-Finals Qualified teams:

USM Alger (Algeria), Zamalek (Egypt), Dreams FC (Ghana), RS Berkane (Morocco), Modern Future (Egypt), Abu Salem (Libya), Rivers United (Nigeria), Stade Malien (Mali).

Tuesday, November 7, 2023

KOCHA ROBERTO OLIVEIRA AFUKUZWA SIMBA, NI BAADA YA KIPIGO CHA BAO 5-1 KUTOKA KWA YANGA!!!

Klabu ya Simba SC imetangaza kuachana na Kocha wake Mbrazil, Roberto Oliveira Gonçalves do Carmo 'Robertinho' (63) baada ya miezi 10 tu kazini tangu alipowasili Januari 13, mwaka huu akitokea klabu ya Vipers ya Uganda.Taarifa ya Simba SC mchana huu imesema kwamba pamoja na Robertinho, pia kocha wa Fiziki, Mnyarwanda Cornoille Hategekimana naye ameondolewa na kwamba hivi sasa kitakuwa chini ya Mspaniola, Daniel Cadena aliyekuwa kocha wa makipa ambaye atafanya kazi pamoja na kocha wa timu za vijana, Suleiman Matola.
Simba SC imeachana na kocha mkuu Roberto Oliveira kufuatia kichapo cha mabao 5-1 kutoka kwa wapinzani wao Young Africans (Yanga SC) katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Jumapili. Wekundu hao wa Msimbazi wamethibitisha katika taarifa yao kuwa wamefikia makubaliano ya kuachana na kocha huyo wa zamani wa Vipers SC sambamba na mkufunzi Corneille Hategemikana mara moja.

"Uongozi wa Simba unapenda kuwashukuru Oliveira na Hategemikana kwa mchango wao kwa timu wakati wa kukaa kwao na kuwatakia kila la kheri katika majukumu yao yajayo." Taarifa hiyo iliendelea kusema: “Tunapoendelea kutafuta kocha mpya, sasa timu itakuwa chini ya kocha Daniel Cardena akisaidiwa na Seleman Matola. Simba ilipata kipigo kizito zaidi dhidi ya wapinzani wao Timu ya Mwananchi kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Saturday, November 4, 2023

KOCHA ERIK TEN HAG ASEMA USHINDI HUU WA LEO DHIDI YA FULHAM ANAUNGWA MKONO

Kocha wa Man United Erik ten Hag amesisitiza kuwa anaungwa mkono na timu yake baada ya ushindi wa 1-0 wa Mashetani Wekundu dhidi ya Fulham
na kutoa wito wa 'njaa, shauku na hamu' kutoka kwa wachezaji wake.
Teg Hag anasema michezo  mitatu ijayo ya Ligi kuu ndiyo itawaonesha wako nafasi ipi katika msimamo wa ligi na inabidi washinde michezo hiyo.

BONDIA YUSUF CHANGARAWE ATWAA MEDALI YA FEDHA


Changalawe na Rais wa TBF

Na Rahel Pallangyo
BONDIA wa Tanzania, Yusuf Changarawe amepata medali ya fedha baada ya kushindwa pambano lake la fainali la mashindano ya kusaka nafasi ya kushiriki Michezo ya Olimpiki itakayofanyika Paris, Ufaransa 2024.

Changarawe alipigwa na bondia kutoka Misri, Abdelrahman Abdelgawwad katika pambano la uzito wa kilo 80 na hivyo kukosa nafasi ya kuiwakilisha Afrika katika Michezo ya Olimpiki.

Bondia huyo na wengine wa Tanzania sasa watasubiri mashindano mengine mawili yatakayofanyika Italia na Thailand Februari na Aprili mwakani ili kusaka tena nafasi ya kwenda Paris katika Olimpiki.

Tanzania katika mashindano hayo ya kufuzu huko Dakar, Senegal ilipeleka mabondia sita, wanne wa kiume na wawili wa kike, ambao walikwenda kusaka nafasi ya kwenda Paris.

Mbali na Changarawe, mabondia wengine wa Tanzania ni Musa Malegesi (kilo 92), Mwalami Salum (kilo 57) na Abdallah Mohamed (kilo 51) wakati wanawake ni Zulfa Macho (kilo 50) na Grace Mwakamele (kilo 60).

Mkuu wa msafara wa timu hiyo alikuwa Rais wa Shirikisho la Ndondi Tanzania (BFT), Lukelo Wilillo. Viongozi wengine ni Mashaga (kocha msaidizi), Samuel Kapunga (Kocha Mkuu) na Aisha George (matroni).

PREMIER LEAGUE: FULHAM 0-1 MANCHESTER UNITED, BRUNO FERNANDES AOKOA JAHAZI KWA TEN HAG


Bruno Fernandes akishangilia kufunga bao lake na wenzake baada ya kuipatia ushindi dakika za lala salama kwenye uwanja wa Craven Cottage, Kocha Erik ten Hag ushindi huu alikuwa akiuhitaji baada ya kuandamwa na vipigo vya mara kwa mara.  ushindi huu unaipandisha Man United nafasi ya 7 wakiwa na alama 18.


Wachezaji wa United wakimpongeza mwenzao Bruno baada ya kufunga bao la dakika za majeruhi na kujizolea alama zote tatu, United wakirejea kutoka kupoteza 3-0 dhidi ya majirani zao Man City.

NBC PREMIER LEAGUE: KAGERA SUGAR 2 vs 1 TANZANIA PRISONS


Timu ya  Kagera Sugar imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Mabao ya Kagera Sugar yamefungwa na Obrey Chirwa kwa penalti dakika ya 20 na Cleophace Mkandala dakika ya 68, wakati bao pekee la Tanzania Prisons limefungwa na Khamis Mcha dakika ya 72.
Kwa ushindi huo, Kagera Sugar inafikisha pointi 12 na kusogea nafasi ya saba, wakati Tanzania Prisons inabaki na pointi zake saba nafasi ya 14 katika ligi ya timu 16 baada ya wote kucheza mechi tisa.



Saturday, October 14, 2023

LIGI YA NBC CHAMPIONSHIP LEAGUE YALAMBA UDHAMINI MNONO



Na Rahel Pallangyo

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeingia mkataba wa miaka mitatu na TV 3 wenye thamani ya Sh. Milioni 613, kwa ajili ya haki za kurusha NBC Championship League.
Udhamini wa TV 3 umekuja siku chache baada ya kupata mdhamini mkuu ambaye ni benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ikiwa ni miaka 11 imepita bila mdhamini.
Akizungumza kwenye hafla hiyo iliyofanyika Dar es Salaam, Rais wa TFF Wallace Karia alisema wameingia mkataba wa kuonesha mubashara NBC Championship League kwa sababu inawasaidia kila kitu kuwa hadharani na kupunguza malalamiko yasiyo na msingi.

Alisema watafanikiwa kuona timu ambazo zinatumia mambo maovu kwa ajili ya kujinufaisha lakini pia kubaini malalamiko ya timu zinazolalamika kufanyiwa maovu na kuwataka viongozi wa klabu kutumia fursa hiyo kujitafutia wadhamini binafsi.
“Nina imani wadhamini wetu hao hawatajutia kabisa kufanya kazi na TFF na nitahakikisha wanapata kipaumbele inapotokea fursa nyingine,"
Karia alisema ligi hiyo ni kati ya ligi ngumu nchini na kuishukuru serikali kwa kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wa ndani.


"Kuonesha kwa Ligi Kuu kupitia Azam TV imekuwa hamasa kubwa kwa kuifanya iwe bora, matarajio yangu kwa mkataba huu tulioingia na TV 3 kwa ajili ya kuonesha mechi ya Championship itafanya pia kuwa bora zaidi na kuleta wadhamini wengine,” alisema Karia.
“Tutakuwa wakali kwa klabu ambazo hazijajianda kucheza daraja la juu, niwaombe wapambane kutafuta wadhamini ili kujimudu katika ligi wanayoshiriki, TFF sio kazi yao kuwatafutia klabu wadhamini,” alisema.
Naye Msimamizi wa vipindi wa TV3, Emmanuel Sikawa alisema mkataba huo ni hatua kubwa kwao kwa sababu wanatarajia kuonesha mechi 170 kati ya 240 ambazo zitachezwa katika ligi hiyo.
Alisema ligi hiyo itaonueshea katika chanel mbili ambazo ya 197 kwa upande wa Dish na 131 kwa Antena, ambazo zinaruka nchi saba.
“Tunatarajia ligi itaoneshwa katika mataifa hayo saba ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda , Afrika Kusini, Uganda, Burundi na Msumbiji ikiwa ni lengo la kutangaza ligi hii na wachezaji kuonesha vipaji vyao na kuonekana kujiuza kwa kutazamwa,” alisema Sikawa.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa TFF na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB).

DK NDUMBARO AMPONGEZA KARIA, WAKISAINI MKATABA NA SANDALAND FASHION WEAR LTD




Na Rahel Pallangyo

SERIKALI imepongeza uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kuingia mkataba wa miaka mitano na Kampuni ya Sandaland Fashion Wear LTD wenye thamani ya Sh bilioni 3 kwa ajili ya kuzivalisha timu zote za Taifa.

Pongezi hizo zilitolewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro, Dar es Salaam juzi baada ya kushuhudia utiaji saini wa mkataba huo.

“Nashukuru sana uongozi wa TFF chini ya uongozi wa ndugu yangu Wallace Karia, ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, TFF inaingia mkataba na mtengenezaji jezi kwa ajili ya timu zote za Taifa, tunaweza kulichukulia jambo hilo kama dogo sana lakini halijawahi kufanyika na linafanywa na TFF chini ya jemedari Wallace Karia,”

“Nasisitiza haya kwa sababu sisi Watanzania ni wazuri sana wa kukosoa lakini tunakuwa wachoyo kusifia pale jambo zuri linapofanyika na kwa mara ili timu zote za taifa ziwezi kupata jezi rasmi zinazotengenezwa na kampuni yenye heshima kubwa hapa Tanzania,” alisema Dk Ndumabaro.

Naye Rais wa TFF Wallace Karia alisema mkataba huo utahusisha timu zote za Taifa na katika mkataba huo watakuwa wanapewa jezi bure kwa timu zote na watakuwa wanapata fedha.

“Leo tunatimiza ahadi yetu ya kuongeza wadhamini zaidi. Mkataba huu ni wa kihistoria kwani tutakuwa tunapata jezi bure na pia tunapata fedha jambo halijawahi kutokea,” alisema Karia.

Pia Karia alisema huo ni utekekezaji wa maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kutaka wawekezaji wazawa kupewa nafasi zaidi ambapo alisema atakuwa anawalegezea kwenye kodi.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Sandaland Fashion Wear LTD, Yusuph Yenga alisema kampuni hiyo ina uzoefu wa kutengeneza jezi na kuahidi kuwa jezi hizo zitakuwa na ubora na viwango vya hali ya juu.

Mkurugenzi wa Tume ya Ushindani (FCC), William Erio alipongeza TFF kwa mafanikio waliyopata katika kipindi cha uongozi wa Karia.

“Sisi Tume ya ushindani ni kuhakikisha wafanyabiashara wanafanikiwa kwa kuweka mazingira mazuri na nimefurahi kuona kampuni ya wazawa imeshinda zanuni ya kutengeza jezi za timu za Taifa,”

MSANII WA MUZIKI BARNABAS ELIAS BALOZI WA HAKIMILIKI


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro akimkabidhi Cheti cha Utambulisho Msanii Barnaba Elias ambaye ameteuliwa kuwa Balozi wa Hakimiliki Tanzania kwenye hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya COSOTA na Bodi ya Bodi Filamu Septemba 12, 2023 Jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo limehudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Hamis Mwinjuma, Katibu Mkuu, Saidi Yakubu na Viongozi wa Taasisi hizo na Mashirikisho ya Sanaa.

DK NDUMBARO AZINDUA BODI MBILI, AZIPA JUKUMU LA KUONGEZA MAPATO


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro akizungumza kwenye hafla ya kuzindua bodi za COSOSTA na Bodi ya Filamu.

Naibu Waziri Hamis Mwinjuma

Katibu Mkuu Said Yakubu

Waziri Dk Ndumbaro, Naibu Hamisi Mwinjuma, Katibu Mkuu, Said Yakub na wajumbe wa bodi za COSOSTA na Bodi ya Filamu

Na Rahel Pallangyo
Wajumbe ya Bodi ya Hakimiliki Tanzania (COSOSTA) na Bodi ya Filamu Tanzania wametakiwa kuhakikisha sekta ya sanaa inatoa ajira za kutosha na wananchi wanafaidi matunda ya kazi zao.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro wakati akizindua bodi za taasisi hizo Dar es Salaam leo

“Wizara hii ina dhamana kubwa na watekelezaji wa kazi zake ni taasisi zinazosimamiwa na Bodi, kazi yenu ni kuhakikisha taasisi mnazozisimamia zinakua kiuchumi ili kukuza Pato la Taifa na uchumi wa wadau wa sekta yetu ya Sanaa ambayo imekua kwa asilimia 19 ”amesisitiza Waziri Dkt. Ndumbaro.

Awali akimkaribisha Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Damas Ndumbaro kuzindua Bodi hizo, Naibu Waziri, Hamis Mwinjuma amewahimiza wajumbe wa bodi hizo kutekeleza wajibu wao ili kuleta uhalisia na utofauti wa utendaji wa kazi wa taasisi hizo kabla ya uteuzi na baada ya kuingia madarakani.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Saidi Yakubu amesisitiza kuwa sekta ya Sanaa nchini imekuwa na Tanzania ni ya pili Afrika ambapo inazalisha filamu 2000 kwa mwaka sawa na wastani filamu sita kwa siku.

Ameongeza kuwa Sekta hiyo imefanikiwa kuzalisha wingi wa filamu na kuwahimiza wajumbe hao kushirikiana na taasisi wanazoziongoza ili kujikita kuzalisha kazi bora ambazo zitakuwa chanzo adhimu cha mapato kwa wasanii na taifa kwa ujumla.

Aidha, Yakubu amezitaka Bodi hizo kuhakikisha Taasisi zinaongeza ukusanyaji wa mapato kutoka nje ya nchi kupitia kazi za Sanaa ambazo zinazooneshwa katika nje ya mipaka ya Tanzania na kuongeza ushirikiano na Taasisi zenye majukumu yanayofanana nayo.

Wakizungumza kuhusu uzinduzi wa Bodi hizo, Mwenyekiti wa Bodi ya Hakimiliki Tanzania (COSOSTA) Victor Tesha na Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Dk. Mona Mwakalinga wamesema watahakikisha linakuwepo jukwaa ndani la kuonesha na kusambaza kazi za Sanaa ndani na nje ya nchi kama ilivyo majukwaa mengine na kusisitiza watasimia kuongeza ubora katika filamu za Tanzania ili zipate soko kubwa zaidi duniani.

RAIS SAMIA AIZAWADIA TAIFA STARS MILIONI 500/=


Rais Samia Suluhu Hassan, ametimiza ahadi ya kutoa Sh. milioni 500 ambazo aliahidi endapo timu hiyo itafuzu kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2023 nchini Ivory Coast.
"Mtakumbuka wakati wa kujiandaa na mechi ya Uganda kule nyumbani, Rais alitoa ahadi ya kutoa Shilingi milioni 500, timu ikifuzu. Nafurahi kuwaambia kwamba hizo fedha sio tu kwamba zitatolewa, zimekwisha letwa Wizarani kwa ajili yenu”, alisema Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Saidi Yakubu, wakati
akizungumza na Wachezaji na viongozi wa timu hiyo jana Septemba 7, 2023 nchini Algeria.

Pamoja na kuwaambia habari hiyo njema, Katibu Mkuu aliwapongeza wachezaji na benchi la ufundi kwa kazi kubwa waliyofanya akisema safari ya matokeo hayo haikuwa nyepesi hadi dakika ya mwisho.

UKARABATI WA BANDARI YA BUKOBA WAENENDELEA KWA KASI


Picha Mbalimbali za Ukarabati wa Bandari mjini Bukoba, kwa upanuzi pamoja na Ujenzi wa Gati ya Kisasa kwa ajili ya Meli kubwa mpya unaendelea katika Manispaa ya Bukoba na mpaka sasa Kazi imefikia hatua hii














Friday, December 9, 2022

FISTON KALALA MAYELE MCHEZAJI BORA WA LIGI KUU TANZANIA NBC, JUMA MGUNDA WA SIMBA KOCHA BORA MWEZI NOVEMBA 2022


Mshambuliaji wa Yanga, Fiston Kalala Mayele ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara mwezi Novemba, huku Juma Mgunda wa Simba akibeba Tuzo ya Kocha Bora.

Wednesday, November 30, 2022

IHEFU YAZIMA REKODI YA YANGA KUTOFUNGWA MECHI YA 50


WENYEJI, Ihefu SC wamezima wimbi la Yanga kutopoteza mechi katika mchezo wa 50 baada ya ushindi wa 2-1 leo Uwanja wa Highland Estate huko Mbarali mkoani Mbeya.

Haukuwa ushindi mwepesi, kwani ilibidi Ihefu watoke nyuma baada ya Yanga kutangulia na bao la Mchezaji Bora wa Ligi Kuu, kiungo Mkongo Yanick Bangala Litombo dakika ya tisa.

Kiungo Mzimbabwe, Never Tigere aliifungia Ihefu SC bao la kusawazisha dakika ya 39, kabla ya Lenny Kissu kufunga la ushindi dakika ya 62. Kwa ushindi huo wa pili tu wa msimu kwa Ihefu iliyorejea Ligi Kuu baada ya msimu mmoja tangu ishuke, inafikisha pointi 11 katika mchezo wa 14 na kusogea nafasi ya 13 kwenye ligi ya timu 16.

Yanga pamoja na kupoteza mchezo huo inaendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi zake 32 za mechi 13 sasa, ikiizidi wastani wa mabao tu Azam FC ambayo pia imecheza mechi moja zaidi.

Sunday, November 25, 2018

FULL TIME: KAGERA SUGAR 1 vs 2 YANGA, RAPHAEL DAUDI AIPA AIPANDISHA YANGA NAFASI YA PILI LEO KAITABA.

Kikosi kilichoanza cha Timu ya Kagera Sugar
Kikosi cha Yanga kilichoanza
Timu ya Yanga wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sugar leo katika Uwanja waKaitaba, Bukoba. 
1-1


Tuesday, May 29, 2018

SIMBA YAKABIDHIWA MILIONI 100 NA SPORTPESA

MABINGWA wa Tanzania klabu ya Simba imekabidhiwa hundi ya Sh. Milioni 100 na kampuni ya SportPesa Tanzania baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
SportPesa Tanzania, ambao pia ni wadhamini wa mahasimu wa Simba, Yanga na Singida United imetekeleza kipengele cha mkataba wao kinachosema timu itakayotwaa ubingwa wa Ligi Kuu itapewa kiasi hicho cha fedha.
Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za kampuni hiyo, Oysterbay, Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa kampuni hiyo, Abbas Tarimba aliwapongeza viongozi na wachezaji wa Simba kwa kutwaa ubingwa kwani wameitendea haki nembo ya SportPesa
“Awali ya yote niwapongeza viongozi na wachezaji wa Simba kwani mmewapa heshima kubwa wana msimbazi kote nchini na kubwa zaidi ni heshima mliyotupa sisi kama wadhamini wenu wakuu, Simba imeitendea haki nembo yetu ya SportPesa na kampuni inaamini kuwa wadhamini wakuu imekuwa ni moja ya chachu iliyosababisha Simba kuchukua ubingwa huu,” alisema Tarimba
“Tunachokifanya leo ni kutimiza moja ya ahadi tuliyotoa wakati tunasaini mkataba Mei mwaka jana kuwa tutatoa bonasi ya Sh Milioni 100 endapo mojawapo ya timu tunazozidhamini itachukua ubingwa wa Ligi Kuu, hivyo bila shaka timu ni Simba”, aliongeza Tarimba
Pia Tarimba amewataka viongozi kupeleke kikosi kamili kwenye michuano ya SportsPesa Super Cup inayotarajia kuanza Juni 3-10 nchini Kenya ili iweza kuwa bingwa na kurudi na kitita cha dola za Kimarekani 30,000 pamoja na kupata nafasi ya kwenda nchini Uingereza kucheza na Everton FC ya Ligi Kuu ya England Uwanja wa Goodison Park.
Naye Kaimu Makamu wa Rais wa Simba, Iddi Kajuna aliishukuru SportPesa kwa kuleta mabadiliko kwenye soka nchini ambapo wao wameyaona kwa upande wao.
“Niwashukuru SportPesa kwa kuleta mabadiliko ya soka nchini ambayo sisi Simba tumeyaona na tutaendelea kutoa ushrikiano katika miaka mingine minne iliyosalia kwenye mkataba wetu”, alisema Kajuna
Simba ni miongoni mwa timu nne kutoka Tanzania zitakazoshiriki michuano ya SportPesa Super Cup itakayofanyika nchini Kenya kuanzia Juni 3-10 ambayo yatashirikisha timu nane
Timu nyingine ni Yanga, Singida United na JKU ya Zanzibar, kutoka Kenya ni timu za Gor Mahia, AFC Leopards, Kakamega Home Boys na Kariabangi Sharks za Kenya. Gor Mahia ndiye bingwa mtetezi wa michuano hiyo baada ya kuwafunga watani wao wao jadi, AFC Leopard katika fainali mwaka jana zilizofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

SIMBA WALIVYOKABIDHIWA MWALI WAO

MABINGWA wapya wa Ligi Kuu Bara Simba,jana walikabidhiwa ubingwa wao na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania John Magufuri katika uwanja wa Taifa Dar es saam.
Simba walitwaa ubingwa huo,licha ya kupoteza mchezo wake wa kwanza kwa bao 1-0 mbele ya Magufuri,hivyo kuvunjia rekodi yake ya kutopoteza mchezo katika Ligi hiyo.
Mshambuliaji Edward Christopher ndiye aliyefunga bao hilo wakati mpira ukielekea ukingoni kunako dakika ya 85,kabla ya Simba kupata penalti dakika ya 93 iliyopigwa na Emmanuel Okwi na Juma Kaseja kupangua.
Aidha,Mgeni rasmi wa mchezo huo,Rais Magufuri aliwapongeza Simba kwa kutwaa ubingwa huo na kuwasihi kuendelea kupambana ikibidi watwae ubingwa wa Afrika.
Akizungumza kabla ya kukabidhi ubingwa huo,alisema Mabingwa hao walistahili kuchukua ubingwa huo,kutokana na namna walivyopambana,lakini hakusita kuipongeza Kagera Sugar kwa kuonesha mchezo mzuri.
Magufuri aliipongeza Wizara husika na uwongozi wa TFF kwa kazi nzuri ambayo inaendelea kuifanya katika kuhakikisha mpira wa Tanzania unakuwa kila siku.
Pia alizungumzia ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa katika Jiji la Dodoma,ambapo alisema Serikali ipo katika mchakato huo na kuongeza matukio ya ajabu kama kung’oa viti hayapaswi kujirudia tena.




Ameziomba Halmashauri kutenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanja na kuomba visimamiwe kwa ubora wa hali ya juu kuhakikisha havivamiwi na mtu yoyote.
Naye,Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe, alisema uwanja wa Taifa ndiyo utakaotumika katika michuano ya AFCON kwa vijana wenye umri wa miaka 17 itakayofanyika mwakani katika ardhi ya nyumbani. Alisema uwanja huo na ule wa uhuru,vinahitaji marekebisho ya hali ya juu ili kuviweka sawa kabla ya michuano hiyo kuanza mwezi Aprili 2019.

COASTAL UNION YAMTUNUKU TUZO WAZIRI UMMY MWALIMU

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) kushoto akipokea tuzo ya heshima ya kutambua mchango wake kwa kuipandisha timu ya Coastal Union kucheza Ligi kuu msimu ujao kutoka kwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Klabu hiyo Salimu Bawaziri mapema leo kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani mjini Tanga wakati alipofungua mashindano ya Ligi ya Banda Cup . Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) katika akionyesha waandishi wa habari tuzo aliyokabidhiwa na klabu ya Coastal Union kwa kutoa mchango wake kuipandisha kucheza Ligi kuu msimu ujao kushoto ni Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Shinyanga (CCM) Azzah Hamadi Hilali Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM)kushoto akipokea cheti kutoka kwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Klabu ya Coastal Union Salim Bawaziri ikiwa ni kutambua mchango wake wa kuisaidia timu hiyo kuweza kupanda daraja kucheza ligi kuu msimu ujao tuzo hiyo walikabidhiwa pia Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Mazingira na Muungano January Makamba ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bumbuli(CCM) na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani(CCM),Asas ya Iringa na Mo Dewji.