Uzinduzi huo ulipambwa na burudani kabambe kutoka kwa Hisia, G Nako, Jambo squad wote kutoka Arusha, Naaziz kutoka Kenya, na Nakaaya mwenyewe yote.hiyonikumpasapotimsaniimwanzao. Akizungumza kwa furaha mwanadada Nakaaya Sumari alisema kuwa anawashukuru sana wote waliokuja kumuunga mkono katika uzinduzi wake. “Nawashukuru sana mashabiki wangu kwa kunipa sapoti ya nguvu kwani wa lijitokeza kwa wingi, nimefurahi sana kwani huu ni mwanzo mzuri,” alisema Nakaaya.
“Albam hii imebebwa na wimbo wa Blessing ambao ni maalum kwa mwanangu kipenzi kwani yeye ni Baraka kwangu hata napokua mbali naye bado nakua na matumaini na faraja,” Nakaaya aliongeza kwa msisitizo. Albam ya Blessing ipo sokoni sasa na inanyimbo nzuri za kuelimisha, kuburudisha na kuliwaza kama vile Utu uzima dawa, Temana na watu, Blessing, Beautiful, I am an African, Sister sister, Ngufurie, na Mwanamke shujaa, kubwa ni kumpa sapoti kwa kununua albam hii.
No comments:
Post a Comment