Sunday, May 20, 2012

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: CHELSEA BINGWA, WAIPOTEZA BAYERN MUNICH KWENYE PENATI. FURAHA YA CHELSEA KILIO CHA SPURS KUTOCHEZA EUROPA LIGI !!! FURAHA YA CHELSEA YAANZIA HAPO HAPO UWANJANI ALLIANZ ARENA!!!

First prize in show: Either Bayern Munich or Chelsea will lift the Champions League trophy after the gameBLUE-TIFUL ... Chelsea players and staff celebrate with the trophy on the pitch
Chelsea imeibuka Klabu Bingwa ya Ulaya baada ya kuibwaga Bayern Munich Uwanja wa nyumbani kwao Allianz Arena kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa Mikwaju ya Penati 4-3 hapo jana kufuatia Mechi hiyo kuwa sare 1-1 katika Dakika 90 na Dakika 30 za nyongeza kutozaa lolote.
Chelsea imeibuka Klabu Bingwa ya Ulaya baada ya kuibwaga Bayern Munich Uwanja wa nyumbani kwao Allianz Arena kwenye Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa Mikwaju ya Penati 4-3 hapo jana kufuatia Mechi hiyo kuwa sare 1-1 katika Dakika 90 na Dakika 30 za nyongeza kutozaa lolote.Fancy display: A mock Champions League trophy was displayed on the pitch as the sides walked out
  STRIKE A POSE ... Chelsea and Bayern Munich teams line up before the matchHata hivyo Bayern Munich watajililia wenyewe kwa kutotwaa Taji baada ya kutawala Mechi yote na kukosa nafasi nyingi za wazi ikiwemo penati ya Arjen Robben mwanzoni tu mwa muda wa nyongeza wa Dakika 30 ambayo iliokolewa na Kipa wa Chelsea Petr Cech.
 Kings of Europe: Chelsea will aim to deny Bayern Munich a fifth crown with victory on the German side's ground
MAKING A STAND ... Bayern fans hold up signs saying 'Our City, Our Stadium, Our Cup'
Bila shaka Chelsea watamkumubuka sana Straika Didier Drogba ambae alisawazisha bao Dakika ya 88 na kufunga Penati ya mwisho iliyowapa ushindi.Friends for now: Chelsea and Bayern Munich fans were in good spirits earlier in the day
At last: Chelsea raise the Champions League Trophy for the first time in their history after Didier Drogba's penalty sealed victory in Munich
Chelsea walikabidhiwa Kombe lao ambalo Nahodha John Terry, aliekuwa kifungoni, na Nahodha wa Mechi hiyo, Frank Lampard walilipokea kwa pamoja na kuamsha shamrashamra kubwa na furaha isiyo kifani iliyowaacha Mashabiki wa nyumbani wa Bayern Munich wakiwa wameduwaa na kulikumbuka pigo walilopewa na Timu nyingine ya England, Manchester United, ambao waliwatandika bao 2-1 Dakika za majeruhi kwenye Fainali ya Mwaka 1999 huko Nou Camp, Barcelona.
 What might have been: Chelsea's suspended skipper John Terry looks on inside the ground
GOLDEN OLDIES ... John Terry and Frank Lampard
John Terry na Frank Lampard
 
Mbali ya kubeba Kombe, Wadau wa Chelsea sasa watamtupia macho Mmiliki wa Klabu, Roman Abramovic, ili kujua nini hatima ya Meneja wa Muda Roberto Di Matteo na nini kitamkuta Didier Drogba, Mwenye Miaka, 34 kwani Mkataba wake ndio unamalizika.
how did Didier Drogba rate?
Drogba hapa alisababisha penati na mkwaju huo ukadakwa!
So far, so good: Chelsea boss Roberto Di Matteo watched his side weather a first half storm from Bayern Munich
Shujaa wa Chelsea ni Didier Yves Drogba ambaye pamoja na kufunga penalti ya mwisho ya ubingwa, pia alifunga bao la Chelsea ndani ya dakika 90. Lakini pia, sifa zimuendee kipa Petr Cech aliyecheza penalti mbili za Bayern. 
GOTTA HAND IT TO 'EM ... Didier Drogba celebrates his leveller
... Didier Drogba akishangilia dakika ya 90 baada ya kutupia nyavuni
Wengine waliofunga penalty za Chelsea ni David Luiz, Frank Lampard na Ashley Cole, wakati Juan Mata yake iliokolewa Neur. Kwa upande wa Bayern, waliofunga ni Lahm, Gomez na kipa Neur.
Lilikuwa bonge la fainali na timu hizo zilimenyana vikali. 

Didier Drogba scores the winning penalty in Munich
                    ... Didier Drogba akifunga akifunga goli la mwisho la penati na kuibuka washindi
Hadi mapumziko hakuna timu iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake, Bayern wakitawala zaidi mchezo na kupata kona kibao, lakini safu ya ulinzi ya Chelsea iliyoongozwa na David Luiz ilikuwa imara kuwadhibiti The Bavarians. 
Chelsea's David Luiz tussles with Mario Gomez
David Luiz na Mario Gomez kazini
Kipindi cha pili Chelsea nao waliamua kuongeza kasi ya mashambulizi na kupata kona tatu, lakini walikuwa ni Bayern Munich waliotangulia kuwainua vitini mashabiki wao, dakika ya 83 kwa bao la Thomas Mueller, aliyeunganisha kwa kichwa cha kudundisha chini krosi ya Toni Kroos na mlinda mlango wa The Blues, Petr Cech akashindwa kuokoa. 

Passion: Fans from both teams show their support inside the stadium pre-matchMASHABIKI WA CHELSEA 
 Passion: Fans from both teams show their support inside the stadium pre-matchMASHABIKI WA BAYERN MUNICH
Kings of Europe: Chelsea celebrate with the Champions League trophy Mara tu baada ya bao hilo, Kocha wa Muda wa Chelsea, Roberto Di Matteo, alimuinua mshambuliaji Fernando Torres kwenda kuchukua nafasi ya Solomon Kalou, jambo ambalo liliongeza uhai wa safu ya ushambuliaji ya Blues.

Alikuwa ni mshambuliaji ambaye anacheza mechi yake ya mwisho na jezi ya Chelsea, Didier Yves Drogba aliyeisawazishia bao timu yake dakika ya 88, kwa kichwa kikali akiunganisha kona iliyochongwa na Juan Mata. 
The moment of victory: Chelsea celebrate a remarkable European triumph as Didier Drogba performs an impromptu dance (below)
Bao hilo liliwanyamazisha malefu ya mashabiki wa Bavarians walioamini Mueller kamaliza kazi na Kombe linabaki Munich- na tangu hapo timu hizo zilishambuliana kwa zamu hadi kipyenga cha kuhitimisha dakika 90 na mchezo kuhamia kwenye dakika 30 za nyogeza. 
No chance: Manuel Neuer failed to stop didier Drogba's bullet header, with David Luiz grabbing his team-mate in celebration (below)
Katika dakika ya tatu ya muda wa nyongeza, Drogba alimkwatua kwa nyuma kwenye eneo la hatari Frank Ribery na refa akawapa penalti Bayern sambamba na kumpa kadi ya njano mshambuliaji wa Ivory Coast. 
On a high: Drogba
Arjen Robben alikwenda kupiga penalti dakika ya 94 na kipa Petr Cech aliyesema mapema amekwishasoma hatua za wachezaji wa Bayern wakati wa upigani wa penalti, alidhihirisha hilo kwa kupangua mkwaju wa winga huyo wa kimataifa wa Uholanzi.
Cech ambaye kesho anasherehekea miaka 30 ya kuzaliwa kwake, hakupangilia mbali mpira huo, ilikuwa jirani mno na yeye na akaugeukia haraka na kuuficha kwenye himaya yake.
Baada ya hapo, timu hizo zilishambuliana kwa zamu na kwa tahadhari mno na hadi dakika 15 za kwanza zinamalizika ubao wa matokeo ulibaki kusomeka 1-1. 

Missed opportunity: Arjen Robben saw his weak penalty saved by Petr Cech in extra-time
Dakika ya 107, Daniel Van Buyten alipata nafasi nzuri akiwa anatazamana na kipa Cech, lakini shuti lake la chini lilikwenda nje sentimita chache upande wa kuliwa wa kipa huyo wa Chelsea. Huna sababu ya kutosema lilikuwa bao la wazi walikosa Bayern.
 Holding on: Petr Cech denies Bastian Schweinsteiger
Dakika ya 111 tena Bayern walifanya shambulizi kali langoni mwa Chelsea, lakini Luiz akaokoa na kuna iliyokwenda kupigwa na Robben, lakini ikaondoshwa kwenye hatari. 
Clearing his lines: Petr Cech takes no chances with a Bayern cornerAgainst all odds: Didier Drogba headed a dramatic equaliser for Chelsea
Watching brief: Suspended Chelsea captain John Terry observed matters from the stands
Chelsea captain John Terry akifatilia kwa makini sana na huku akiangalia akiwa amesimama!

In attendance: Roman Abramovich watches Chelsea in Munich
Roman Abramovich naye alikuwepo akiangalia kazi ya vijana wake wa Chelsea - Munich
Dakika 120 zinatimu matokeo 1-1 na katika matuta, Chelsea wakafuta machungu ya 2008 walipofungwa na Manchester United kwenye fainali mijni Moscow.

Quite remarkable: Roberto Di Matteo and John Terry savour victory
 Glory boy: Didier Drogba celebrates after scoring the winning penalty
 Clash: Jerome Boateng and Didier Drogba lie prostrate after an aerial collisionNo way through: Jerome Boateng thwarts Didier Drogba




Look what I bought: Roman Abramovich holds up the trophy
Managing to lift it: Roberto Di Matteo raises the European Cup


Arjen Robben and Mario Gomez look gutted after losingDistraught: Philipp Lahm confronts Bastian Schweinsteiger after the midfielder missed his penaltyThat's football: Drogba consoles Bayern Munich's Bastian Schweinsteiger Fallen: Bayern Munich missed a host of chancesBowed and beaten: Bayern's Bastian Schweinsteiger (right) and head coach Jupp Heynckes




VIKOSI
Bayern Munich: Neuer, Lahm, Boateng, Tymoschuk, Contento, Schweinsteiger, Kroos, Robben, Mueller, Ribery, Gomez.
Akiba: Butt, Van Buyten, Petersen, Olic, Rafinha, Usami, Pranjic.
 ======================================================
Chelsea: Cech, Bosingwa, Luiz, Cahill, Cole, Kalou, Mikel, Lampard, Bertrand, Mata, Drogba
Akiba: Turnbull, Essien, Romeu, Torres, Malouda, Ferreira, Sturridge.
Refa: Pedro Proenca (Portugal)
=====================================================
MIKWAJU YA PENATI:
Phillip Lahm (Bayern)=Afunga 1-0
Juan Mata (Chelsea)=Akosa 1-0
Mario Gomez (Bayern)=Afunga 2-0
David Luiz (Chelsea)=Afunga 2-1
Manuel Neuer (Bayern)=Afunga 3-1
Frank Lampard (Chelsea)=Afunga 3-2
Ivica Olic (Bayern)=Akosa 3-2
Ashley Cole (Chelsea)=Afunga 3-3
Bastian Schweinsteiger (Bayern)=Akosa 3-3
Didier Drogba (Chelsea)=Afunga 3-4

TIMU ZA ENGLAND ZILIZOWAHI KUWA BINGWA WA ULAYA:

Liverpool (Mara 5)
Manchester United (3)
Nottingham Forest (2)
Aston Villa (1)
Chelsea (1)

MATCH FACTS
Bayern Munich: Neuer, Lahm, Boateng, Tymoschuk, Contento, Schweinsteiger, Kroos, Robben, Muller (Van Buyten 86), Ribery (Olic 97), Gomez. Subs not used: Butt, Petersen, Rafinha, Usami, Pranjic.
Booked: Schweinsteiger.
Scorer: Muller 83.
Chelsea: Cech, Bosingwa, Luiz, Cahill, Cole, Kalou (Torres 84), Mikel, Lampard, Bertrand (Malouda 73), Mata, Drogba. Subs not used: Turnbull, Essien, Romeu, Ferreira, Sturridge.
Booked: Cole, Luiz, Drogba, Torres.
Scorer: Drogba 88.
Referee: Pedro Proenca (Portugal).
Attendance: 69,901.

No comments:

Post a Comment