Monday, October 19, 2015

KIPA PETR CECH KUANZA KESHO KWENYE UEFA CHAMPIONS LEAGUE DHIDI YA BAYERN MUNICH. OSPINA NJE! ARSENAL WAKIJIFUA KUJIANDAA NA BAYERN

Alexis Sanchez kwenye mazoezi kujiandaa na Bayern MunichTheo WalcottKipa Petr CechPer Mertesacker akiteta jambo na Meneja wake Arsene Wenger wakati wa MazoeziWakati wazoeziTheo Walcott nae alishiriki kwenye mazoeziGlen Kamala nae kajifua
Petr akidaka mpira leo wakati wa mazoezi, Kesho ndie atayeliona lango dhidi ya Bayern Munich.

Arsenal wamechapwa Mechi zao zote mbili za Kundi F kutoka kwa Dinamo Zagreb na Olympiakos na wapo mkiani mwa Kundi hilo na Mechi zao 2 zinazofuata ni dhidi ya Mabingwa wa Germany Bayern Munich.Calum Chambers na Theo
Ikiwa Arsenal watafungwa na Bayern basi wapo hatarini ya kutofuzu kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL kwa mara ya kwanza katika Miaka 16.
Hii si Mechi rahisi kwa Arsenal kwani Bayern watatinga Jijini London Uwanjani Emirates wakiwa na wimbi la ushindi la Mechi 12 mfululizo.
Lakini hilo halimtishi Wenger ambae amesema: “Sasa tupo katika hali nzuri na mkazo kwetu ni Mechi hii ya Jumanne.”Msimamo ulivyo!
Arsenal hivi sasa wapo kwenye wimbi zuri la ushindi kwenye Ligi Kuu England ambalo limewapaisha hadi Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 tu nyuma ya Vinara Man City.
Mara ya mwisho kwa Arsenal na Bayern kukutana kwenye UCL ni Mwaka Jana walipotoka 1-1 huko Allianz Arena Jijini Munich na Bayern kushinda 2-0 Uwanjani Emirates katika Mechi yao ya kwanza.Mesut OzilCazorla, Alexis Sanchez karibu na Olivier Giroud

No comments:

Post a Comment