Taarifa toka katika website yake ilisema ya kuwa mchezaji huyo hana mpango wa kuongeza mkataba klabuni hapo.
Taarifa hiyo inawafanya Man City kujiweka sawa na kujiandaa ili kuweza kumpata mchezaji huyo kwani wamekuwa wakimfuatilia kwa mda mrefu sasa.
Nimekaa kimya mda wote huu kwa heshima na uzalendo nliokuwa nao kwa klabu na kama tulivyokubaliana na Mr Gazidis na Mr Wenger. Lakini kutokana na habari nyingi zinazoskika katika vyombo vya habari, nadhani ni bora na nyie mashabiki mjue ni nini kinaendelea.
Kutokana na heshima kubwa nliyokuwa nayo kwa Mr Wenger, wachezaji wenzangu na mashabiki sitaki kutoa maelezo zaidi ila kwa kifupi ni kuwa katika mkutano huo ilikuwa wazi mambo waliyokuwa yakiongelewa kuhusu jinsi ya kuiendesha timu ni tofauti na muono wangu nliokuwa nao na hivyo sikukubaliana nao.
Naipenda klabu hii na mashabiki wake. Nimekulia hapahapa Arsenal.
Kila mtu katika klabu hii wamekuwa wakinisaidia daima miaka yote hii na nimekuwa nkijitahidi kurudisha fadhila uwanjani na nje ya uwanja. Ninafuraha sana ya kuwa sehemu ya klabu hii kwa mda wote huu wa miaka minane.
Pindi Mr Gazidis atakaporudi toka likizo yake ya Amerika tutaongea zaidi na baada ya hapo ntawataarifu yatakayokuwa yanaendelea”.
No comments:
Post a Comment