BUKOBA SPORTS

Friday, April 24, 2015

RATIBA - LA LIGA: EL DERBI BARCELONI KUPIGWA JUMAMOSI, ESPANYOL vs BARCELONA, JUMAPILI CELTA VIGO vs REAL MADRID

Ingawa wapo Nafasi ya 10 wakiwa Pointi 36 nyuma ya FC Barcelona, Espanyol bado ni Mahasimu wakubwa wa Vinara hao wa La Liga na Jumamosi Jiji la Barcelona litajaa shamrashamra za 'El Derbi Barceloni'.
Ingawa pia Msimu huu Barca waliinyuka Espanyol 5-1 ndani ya Nou Camp katika Mechi yao ya kwanza ya La Liga, Uwanjani Estadi Cornella-El Prat, Espanyol huwa habari nyingine na Barca wanajua hilo.
Licha ya kuwa hii ni Dabi na huwa zina kawaida ya kutotabirika, Barcelona wapo kwenye presha ya kushinda ili kuendelea kuongoza Ligi kwani wakitetereka tu nyuma yao kwa Pointi 2 wapo Real Madrid.
Real Madrid wao wanacheza Jumapili Ugenini na Celta Vigo Timu ambayo waliichapa 3-0 katika Mechi ya kwanza.
Mabingwa Watetezi Atletico Madrid, ambao Juzi walipigwa 1-0 na Real na kutupwa nje ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, Jumamosi wapo Nyumbani kucheza na Elche wakiwa tayari wameshapoteza matumaini ya kutetea Taji lao.


LA LIGA
RATIBA

Ijumaa Aprili 24

21:45 Cordoba CF v Athletic de Bilbao

Jumamosi Aprili 25
17:00 RCD Espanyol v FC Barcelona
19:00 Atletico de Madrid v Elche CF
21:00 Getafe CF v Levante
23:00 Real Sociedad v Villarreal CF
Jumapili Aprili 26
13:00 Malaga CF v Deportivo La Coruna
18:00 UD Almeria v SD Eibar
20:00 Sevilla FC v Rayo Vallecano
22:00 Celta de Vigo v Real Madrid CF
Jumatatu Aprili 27

21:45 Valencia C.FGranada CF

No comments:

Post a Comment