David de Gea, Miaka 21, ambae alisajiliwa kwa Pauni Milioni 18 kutoka Atletico Madrid mwanzoni mwa Msimu na kumfanya Kipa wa bei ghali huko England, alishaanza kupoteza namba hapo Man United ambayo ilikuwa imekamatwa na Kipa toka Denmark Anders Lindegaard baada ya De Gea kufanya makosa yaliyowapa ushindi Blackburn Mwezi Desemba.
Akizungumzia hilo, Ferguson amesema: ‘Sasa ametulia. Hakuruhusu makosa yake yamchanganye na sasa anacheza kwa kujiamini. Eneo pekee alilokuwa akilaumiwa ni mipira ya juu. Amesimama imara na alijua nini changamoto. Sasa ameshaanza kuzoea Soka la Uingereza!’
No comments:
Post a Comment