Mwanamuziki wa Bongo Flava, Diamond anatarajia kuigiza kama mhusika mkuu kwenye filamu itakayotayarishwa na kampuni ya Selles Business Inc na kusambazwa na Steps Entertainment Limited.
Akiongea kwa simu na Bongo5 jana, mtunzi na muongozaji wa filamu hiyo Selles Mapunda amesema, “mwishoni mwa mwaka jana nilikuwa na wazo la kufanya sinema, nilifanya kikao na Diamond pale Lions Hotel Sinza, tukaongea biashara nyingine, tukaenda kwenye show moja Mombasa na yeye lakini pia likaja wazo la kufanya naye sinema.”
Mapunda amesema ameifanyia kazi filamu hiyo kwa zaidi ya miezi saba na sasa yupo kwenye hatua ya mwisho ya kuikamilisha.
Amesema kwenye filamu hiyo ya Diamond atawashangaza watu kama ilivyokuwa kwenye filamu ya Crazy Tenant aliyoigiza msanii Peter Msechu na Wema Sepetu.
Akiongea kwa simu na Bongo5 jana, mtunzi na muongozaji wa filamu hiyo Selles Mapunda amesema, “mwishoni mwa mwaka jana nilikuwa na wazo la kufanya sinema, nilifanya kikao na Diamond pale Lions Hotel Sinza, tukaongea biashara nyingine, tukaenda kwenye show moja Mombasa na yeye lakini pia likaja wazo la kufanya naye sinema.”
Mapunda amesema ameifanyia kazi filamu hiyo kwa zaidi ya miezi saba na sasa yupo kwenye hatua ya mwisho ya kuikamilisha.
Amesema kwenye filamu hiyo ya Diamond atawashangaza watu kama ilivyokuwa kwenye filamu ya Crazy Tenant aliyoigiza msanii Peter Msechu na Wema Sepetu.
No comments:
Post a Comment