BUKOBA SPORTS

Wednesday, October 17, 2012

LINIAS MHAYA AYAAGA MASHINDANO YA EBSS 2012


Madam Ritha akitoa maoni yake juu ya mshiriki aliyekua juu ya jukwaa Jumapili ya tarehe 15, October 2012 mshiriki mmoja wa EBSS, Linias Mhayaaliyaaga mashindano na hivyo kubaki washiriki tisa tu. Washiriki tisa waliobakia wamegawanywa katika makundi matatu na kila Jaji kapewa washiriki
watatu watakaokuwa chini ya usimamizi wake, majaji wanatakiwa kuwapa
maelekezo kuhusu kuimba na kuwachagulia nyimbo za kuimba.

Godfrey Kato akiingia katika jukwaa

Husna Nassor akiimba jukwaani

Menynah Atick akiimba mbele ya majaji na watazamaji

Salma Yusuph akipiga gitaa

 

SAFARI YA LINIAS KUTIMIZA NDOTO ZAKE ILIANZIA TUSKER PROJECT FAME 5 HUKO NAIROBI

 Linias aliondoka Mwanza tarehe 26 April,2012 na kuelekea Dar es salaam  kwenye Audition za Tusker Project Fame 5 zilizofanyika kesho yake(tarehe 27-28). Akawa miongoni mwa watanzania 4 tu waliochaguliwa kuiwakilisha nchi katika mashindano hayo. Tarehe 18 May akatua Nairobi tayari kwa shughuli hiyo.
.
 Tarehe 19 may, Audition za Top 25 zikafanyika, washiriki 7 akiwemo mtanzania 1 walirudi makwao. washiriki 6 akiwamo Linias wakawekwa kwenye Probation na ilitakiwa waimbe jukwaani siku ya ufunguzi wa mashindano hayo wiki mbili baadaye ili kupata nafasi ya watu 3  kuingia kwenye Academy. Washiriki hao ni Doreen(kenya), Joe(Burundi), Nancy(sudan kusini), Linias(Tanzania), Brian(Uganda) na Diana(Rwanda). Linias alichaguliwa wimbo wa Mbagala wa msanii Diamond.
Kwa kuzingatia kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kwa kijana huyo kuimba jukwaani na mbele ya mamilioni ya watazamaji wa Afrika mashariki, alijitahidi kadri ya uwezo wake kutoa kile alichokuwa nacho. Pamoja na kuimba vizuri, bado Linias hakufanikiwa kupata nafasi kati ya hizo 3 zilizokuwa zimebakia, hivyo safari ya Tusker ikawa imeishia usiku huo. Washiriki waliofanikiwa kuendelea na mashindano ni Doreen, Nancy na Joe. Linias alirejea Tanzania tarehe 4 June mwaka huu na kuelekea Mwanza kujinoa zaidi kwani haikuwa mwisho wa maisha yake kimuziki.

 _____________________________________________________________


WEMA SEPETU NA AUNT EZEKIEL WAWAOMBA RADHI WATANZANIA KWA KUPIGWA PICHA ZA UCHI WAKATI WA TAMASHA LA FIESTA DODOMA.
Mastaa taja hapo juu  wameomba msamaha kwa tendo lao lililoichefua jamii kwa picha zisizositiri miili yao, Akiongea Wema anasema steji ya fiesta iko juu na waandishi wa habari hukaa chini wanapopiga picha huonekana wako uchi. Ingawa suala lao halihitaji maelezo mengi maana washahili wanasema PICHA INAONGEA KULIKO MANENO. Nadhani wamekaa na kupitia picha na kuona ukweli wamejitia aibu na kufedhehesha jamii. Wajitahidi wasirudie yaliyotokea maana ni aibu sana. CHANZO TBC TAIFA!

Moja ya picha ya Msanii Aunty Ezekiel iliyosambaa kwenye mitandao ya Kijamii hivi karibuni wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012.

No comments:

Post a Comment