BUKOBA SPORTS

Friday, October 12, 2012

MCHEZAJI WA MANCHESTER UNITED, ASHLEY YOUNG AREJEA KUANZA NA STOKE CITY.

Manchester, Winga wa Manchester United Ashley Young, ameanza Rasmi kujifua baada ya kuwa Majeruhi wa goti tangu agosti 25, alipoumia kwenye mechi ya ligi kuu dhidi ya Fulham.
Gazeti la "Dailymail" limeeleza  kuwa Young ameanza kujifua muda wote na wachezaji wa kikosi cha kwanza cha United ambao hawapo kwenye majukumu ya ya timu zao za taifa.

Kocha wa Manchester united, Sir Alex Ferguson anatumaini kwamba Young atakuwepo dimbani kwenye mechi ya ligi kuu dhidi ya STOKE CITY, Octoba 20, mwaka huu 2012.

No comments:

Post a Comment