>>GERMANY waongoza 4-0 na kutoka sare na Sweden 4-4!!
>>MABINGWA SPAIN 1-1 na FRANCE!
Mechi
ya Poland na England iliyokuwa ichezwe huko Warsaw
hapo jana
ililazimika kuahirishwa kwa sababu ya mvua kubwa na Uwanja kujaa maji
licha ya Uwanja huo wa kisasa kuwa na Paa ambalo huweza kufungwa na
kufunguliwa lakini, katika hali ya utata, iliamuliwa lisifungwe kabla ya
Mechi wakati utabiri ulikuwa ni wa Mvua kubwa.
Mechi hiyo imepangwa kufanyika leo.
Germany 4 Sweden 4
Germany waliongoza kwa bao 2 ndani ya Robo Saa kwa bao za Moroslav Klose na Sentahafu Per Mertesacker kupiga bao la 3.
Ndipo katika Dakika ya 62, Sweden,
wakiongozwa na Nahodha wao Zlatan Ibrahimovic, wakaanza kurudisha mabao
kwa bao la kichwa la Ibrahimovic kufuatia pasi ndefu ya Kim Kallstrom.
Mikael Lustig akapiga bao moja na Johan Elmander akapiga bao la 3 na kuifanya ngoma iwe 4—3 katika Dakika ya 76.
Germany bado wanaongoza Kundi C wakiwa na Pointi 10 kwa Mechi 4 wakifuatiwa na Sweden wenye Pointi 7 kwa Mechi 3.
Spain 1 France 1
Mchezaji wa France, ambae ni Straika
wa Arsenal, Olivier Giroud, alitoka Benchi na kuifungia bao la
kusawazisha katika dakika za mwisho na kuwafanya kutoka sare na Mabingwa
wa Dunia na Ulaya, Spain, ya bao 1-1 katika Mechi ya Kundi I
iliyochezwa huko Madrid.
Sergio
Ramos ndie aliefunga bao la Spain katika Dakika ya 25 na baadae Kipa wa
France Hugo Lloris, anaedakia Tottenham, aliokoa Penati iliyopigwa na
Cesc Fabregas.
Spain, ambao watarudiana na France Machi
Mwakani huko Ufaransa, bado wanaongoza Kundi hili kwa ubora wa magoli
wakiwa na Pointi 7 sawa na France kwa Mechi 3 kila mmoja.
MATOKEO:
Jumanne Oktoba 16
Russia 1 Azerbaijan 0
Israel 3 Luxembourg 0
Belarus 2 Georgia 0
Andorra 0 Estonia 1
Latvia 2 Liechtenstein 0
Bosnia-Hercegovina 3 Lithuania 0
Czech Republic 0 Bulgaria 0
Romania 1 Netherlands 4
Ukraine 0 Montenegro 1
Cyprus 1 Norway 3
Faroe Islands 1 Rep of Ireland 4
Croatia 2 Wales 0
Hungary 3 Turkey 1
Iceland 0 Switzerland 2
Macedonia 1 Serbia 0
San Marino 0 Moldova 2
Slovakia 0 Greece 1
Austria 4 Kazakhstan 0
Belgium 2 Scotland 0
Germany 4 Sweden 4
Italy 3 Denmark 1
Albania 1 Slovenia 0
Spain 1 France 1
Poland v England [IMEAHIRISHWA KUCHEZWA LEO]
Portugal 1 Northern Ireland 1
FAHAMU:
-ULAYA yapo Makundi 9
-Washindi 9 wa kila Kundi
wataingia Fainali moja kwa moja na Washindi wa Pili 8 bora wenye rekodi
nzuri dhidi ya Timu zilizomaliza nafasi za Kwanza, Tatu, Nne na Tano
kwenye Kundi lao watapelekwa kwenye Droo kupanga Mechi 4 za Mchujo,
zitakazochezwa nyumbani na ugenini, ili kupata Timu nne zitakazoingia
Fainali.
No comments:
Post a Comment