BUKOBA SPORTS

Monday, February 25, 2013

ENGLISH PREMIER LEAGUE: WEST HAM 2 vs TOTTENHAM HOTSPUR 3, GARETH BALE AIPA USHINDI MNONO SPURS ATUPIA 2 AKIWAUA WEST HAM DAKIKA ZA LALA SALAMA, AIPANDISHA HADI NAFASI YA 3!!

LEO, Tottenham wakicheza ugenini Upton Park na West Ham katika Mechi iliyokuwa imesalia ya (BPL), Barclays Premier League, imeifunga timu ya West Ham goli 3-2 na kuweza kupanda hadi nafasi ya tatu kwa kuishusha Chelsea nafasi hiyo ambao jana walichapwa na timu ya Man City goli 2-0.
Tottenham ndiyo ilikuwa ya kwanza kubata bao baada ya mchezaji wao matata Gareth Bale kuachia shuti la pembeni dakika ya 13 na kufanikiwa kupata ushindi hapo uwanjani Uptown Park. Muda mfupi baadaye mchezaji Andrew Carroll akakwatuliwa na Parkerna hatimaye mwamuzi Howard Webb kudai kuwa mpira utengwe penati, Andrew Carroll hakufanya makosa akaachia shuti kali la juu na mpira kuishilia nyavuni mwa Spurs na kufanya 1-1. Kipindi cha kwanza kimeisha kila timu ikiwa na bao moja.
Bale force: Gareth Bale opened the scoring for Tottenham
Gareth Bale akiipatia Tottenham goli dakika ya 13
Paying the penalty: Scott Parker's late foul on Andy Carroll handed West Ham a spot-kick
Scott Parker akimwekea kiatu Andy Carroll hatimaye kuanguka na refa Howard webb kutoa penati
Andrew Carroll akichonga penati hiyo.
Kipindi cha pili kimeanza kwa kila timu kumshambulia mwenzake Spurs wakikosa kosa magoli kwenye lango la West Ham United. West Ham nao wakikosa kosa na kupata kona nyingi, Dakika ya 59 kipindi cha pili mchezaji wa West Ham United Joe Cole akaiongezea bao la pili West Ham baada ya kutuliza mpira vizuri na kuachia shuti lililoenda kwa kudunda dunda na kuweza kumpita kipa wa Spurs Lloris, Goli hili likawapa nguvu West Ham na kuendeleza mashambulizi na kurudi nyuma na huku Spurs wakiangaika kuweza kuziba pengo hilo kwa haraka na kumfanya kocha Andre Villas-Boas kutokaa na kuchanganyikiwa kwa muda. Goli hilo halikuweza kudumu dakika ya 76 mchezaji Gylfi Sigurdsson kutokea benchi akaisawazishia bao hilo timu ya Spurs na kufanya 2-2. Gareth Bale dakika za lala salama dakika ya 90 akaipatia goli la ushindi Spurs. Ushindi huo umewaweka pazuri nafasi ya tatu kwa kuishusha Chelsea chini nafasi ya nne na kupata pointi 51 juu ya Chelsea wenye pointi 49 na kuwaweka nafasi ya 14 West Ham United wakiwa na pointi zao 30. Sasa kazi imebaki kwa nafasi ya nne ikigombaniwa na timu Kadhaa kama Chelsea,Arsenal, Everton pamoja na Liverpool.
Acrobatics: Gareth Bale attempts an overhead kick
Gareth Bale akiwa kwenye kashikashi za kutaka kufunga goli
Frustration: Spurs boss Andre Villas-Boas looks on at Upton Park
kocha wa Spurs Andre Villas-Boas kwenye uwanja wa Upton Park akiwa amepagawa baada ya kufungwa goli la pili.
Gylfi Sigurdsson akishangilia baada ya kupata goli.In front: Joe Cole put West Ham in the lead after latching on to a long ball ushindi mtamu....
Unstoppable: Gareth Bale lets fly late in the day to clinch the match for Tottenham
Gareth Bale akitupia kuipa ushindi Tottenham
Main man: Gareth Bale scored Tottenham's first goal after just 13 minutes
Gareth Baleakiwapatia pointi 3 muhimu sana Spurs
Unbelievable: Gareth Bale rushes to the bench after scoring his stunning match-winning goal
Gareth Bale akishangilia dakika za lala salama baada ya kufunga goli la ushindi na kuipandisha Spurs nafasi ya tatu.
VIKOSI:
West Ham: Jaaskelainen, Reid, O'Brien, Collins, Demel (Pogatetz 72), Nolan (Taylor 35), Jarvis, Diame, J Cole, O'Neil, Carroll
Subs not used: Spiegel, Collison, Taylor, C Cole, Vaz Te, Chamakh
Goals: Carroll 25 (pen), J Cole 58
Booked: Diame, J Cole, O'Neill, Collins
Tottenham: Lloris, Vertonghen, Dawson, Walker, Caulker, Lennon, Parker (Livermore 88), Bale, Holtby (Sigurdsson 56), Adebayor, Dembele (Carroll 75)
Subs not used: Friedel, Gallas, Naughton, Assou-Ekotto, Sigurdsson
Goal: Bale 13, 90 Sigurdsson 76
Booked: Dembele
Referee: Howard Webb
 

RATIBA: BARCLAYS PREMIER LEAGUE

Jumamosi Machi 2
[Saa 12 Jioni]
Chelsea vs West Bromwich Albion
Everton vs Reading
Manchester United vs Norwich City
Southampton vs Queens Park Rangers
Stoke City vs West Ham United
Sunderland vs Fulham
Swansea City vs Newcastle United
[Saa 2 na Nusu Usiku]
Wigan Athletic vs Liverpool
 

Jumapili Machi 3
[Saa 1 Usiku]
Tottenham Hotspur vs Arsenal
Jumatatu Machi 4
[Saa 5 Usiku]
Aston Villa vs Manchester City

No comments:

Post a Comment