BUKOBA SPORTS

Wednesday, September 25, 2013

ATLETICO MADRID YAFUATA NJIA ZA BARCA, WAWAFUKUZIA KWA KARIBU!! MESSI NA NEYMAR WANG'ARA WAKIIFUNGA 4-1 REAL SOCIEDAD!


Lionel Messi
Jana Usiku ilinguruma na zile mbio za kileleni kati ya Mabingwa Barcelona na Atletico Madrid bado zinaendelea kwa kushikana kwa Pointi ingawa Barca wako juu kwa ubora wa Magoli baada Timu zote kushinda Mechi zao.
Wakati Barca wanaichapa Real Sociedad Bao 4-1 na kufikisha Pointi 18 kwa Mechi 6 na Atletico Madrid nao wakaichapa Osasuna Bao 2-1 na kukamata Pointi 18 kwa Mechi 6.
Dynamic duo: Messi and Neymar both netted in a comprehensive 4-1 victory against Real Sociedad
Bao za Barca kwenye Mechi yao zilifungwa na Neymar Dakika ya 5, Lionel Messi, ya 8, Sergio Busquets, ya 23 na Marc Batra, ya 77 huku Bao la Real Sociedad likifungwa na lberto De La Bella katika Dakika ya 64.
Bao za Atletico Madrid zote mbili zilifungwa na Costa na lile la Osasuna na Riera.
La Liga inaendelea tena leo Usiku kwa Real Madrid kucheza Ugenini na Elche pamoja na Mechi nyingine kadhaa.
Huko Germany Mechi za Raundi ya Pili ya German DFB Pokal 2013/2014 zilinguruma na Borussia Dortmund walihitaji Dakika 120 ili kuitoa TSV 1860 Munich baada kutoka 0-0 katika Dakika 90.
Bao za Borussia Dortmund zilifungwa na Pierre‑Emerick Aubameyang kwa Penati ya Dakika ya 105 na Henrik Mkhitaryan katika Dakika ya 107.
Mechi nyingine za German DFB Pokal 2013/2014 zinaendelea leo ambako Mabingwa Watetezi Bayern Munich watacheza na Hannover pamoja na Mechi nyingine kadhaa.
Huko italy, kwenye Serie A, Jana ilikuwepo Mechi moja tu ambayo Udnese iliifunga Genoa kwa Bao 1-0 na Bao la ushindi kufungwa na Calaio katika Dakika ya 79 kwa kujifunga mwenyewe.
Leo Usiku ziko Mechi lukuki za Serie A ambapo pia Mabingwa Watetezi Juventus watakuwa Ugenini kucheza na Chievo Verona na Vinara AS Roma wako Ugenini kucheza na Sampdoria huko Napoli, waliofungana kwa Pointi na AS Roma, wako Nyumbani kucheza na Sassuolo.
RATIBA/MATOKEO
SERIE A
Jumanne Septemba 24
Udinese 1 Genoa 0

Jumatano Septemba 25
[Mechi zote Saa 3 Dak 45 Usiku]
Bologna v AC Milan
Chievo v Juventus
Lazio v Catania
Livorno v Cagliari
Napoli v Sassuolo
Parma v Atalanta
Sampdoria v AS Roma
Torino v Hellas Verona
Alhamisi Septemba 26
Inter v Fiorentina

LA LIGA
RATIBA
Jumanne Septemba 24
Barcelona 4 v Real Sociedad 1
Levante 1v  Valladolid 1
Atletico Madrid 2  v Osasuna 1
Malaga 2  v Almeria 0
Jumatano Septemba 25
2100 Granada v Valencia
2100 Sevilla v Rayo Vallecano
2300 Elche v Real Madrid
Alhamisi Septemba 26
2100 Athletic Bilbao v Betis
2300 Getafe v Celta Vigo
2300 Villarreal v Espanyol

No comments:

Post a Comment