MICHUANO ya kombe la mtoano la Capital One imefanyika jana usiku kwa
Tottenham kuifunga Aston Villa 4-0 huku kukiwa na kituko cha aina yake pale
mshambuliaji wa Aston Villa Nicklas Helenius alipojaribu kwenda kufunga
licha ya kukabwa na beki Jan Vertonghen hadi bukta ikamvuka. Wakati
Helenius anachanja mbuga kuelekea kwenye 18 ya Tottenham Vertonghen
alihofia kuwa mshambuliaji huyu angeweza kusawazisha bao lao la kwanza
lililofungwa na Defoe na hivyo akaamua kumdhibiti kwa kumvuta bukta. 
Nicklas Helenius akikosa mpira wakati Aston Villa wakiumana na Spurs usiku wa kuamkia leo..

...Penati au...! Majanga!

Jermain Defoe akiwapatia bao Spurs na kuongeza mashambulizi

...akishangilia hapa..baada ya kufunga bao

Paulinho aliongeza la pili..!

Nacer Chadli akawaua baada ya ktupia la tatu na kufanya 3-0 dhidi ya Aston Villa
No comments:
Post a Comment