BUKOBA SPORTS

Saturday, September 21, 2013

VODACOM PREMIER LEAGUE: LIVE MATCH: KAGERA SUGAR 3 v ASHANTI UNITED 0 FULL TIME!


Wachezaji pande zote mbili wakisalimiana
Wachezaji wa Kagera Sugar wakiwasalimia wenzao Ashanti United kutoka jijini Dar es Salaam
Salaam zikiendelea uwanjani kabla ya mechi kuanza.

Waamuzi wa mtanange huu wakipata picha ya pamoja hapa.

Kikosi cha Kagera Sugar kilichoanza kumenyana na Ashanti United
Kikosi cha kilichoanza cha Kagera Sugar
Kikosi cha Ashanti United kilichoanza
Waamuzi na timu kapteni pande zote mbili wakiteta kuhusu mtanange huu na kujua uelekeo wa kila timu
Benchi la Ashanti United na viongozi wake
Benchi la Kagera Sugar kulia ni Kocha wake Uganda Jacksony Mayanja akiteta na kiongozi msaidizi Mlage  Kabange kuhusu matanange huu
Mtanange ukiendelea.
Na Faustine Ruta, Bukoba
Bao la kwanza la kagera Sugar limefungwa na kiungo mshambuliaji wa timu hiyo  Daudi Jumanne "Dunga" dakika ya 31 baada ya kupokea krosi nzuri kutoka kwa Suleiman Kibuta.
Dakika ya 68 kipindi cha pili mchezaji aliyekuwa amekosakosa mabao kadhaa Suleiman Kibuta akaipachikia bao la pili baada ya kupita katikati ya mabeki wa timu ya Ashanti United na kutupia nyavuni. Temi Felix akamalizia bao la mwisho dakika ya 89 na kufanya 3-0 dhidi ya timu ya Ashanti United kutoka jijini Dar es salaam.
Kipa wa Ashanti akijionea mwenye timu yao kuzidiwa

Mashabiki
Kocha wa Kagera Sugar akisisitiza jambo uwanjani kuhusu kuziba nafasi zilizokuwa zimeachwa wazi na baadhi ya wachezaji wake.,
Kipa wa Ashanti United akidaka shuti kali kipindi cha pili lililopigwa na Temi Felix

Suleiman Kibuta akishangilia baada ya kufunga bao la pili dakika ya 68 kipindi cha pili.
Wachezaji wa Ashanti Unite kwenye mtanange huu hawakuwa makini sana kwani walicheza mchozo wa rafu sana na baadhi ya wachezaji kuambulia kupewa kadi za njano na kuwaletea tatizo uwanjani wakiepuka kupewa kadi ya pili na hatimaye kutolewa nje.
Furaha kwa mchezaji aliye funga bao la pili na hapa akipongezwa
Hongera sana!!!
Wachezaji wa Kagera Sugar wakipongezana jioni hii baada ya kuifunga bao la tatu na la mwisho kwenye dakika za majeruhi dakika ya 89 kipindi cha pili.

No comments:

Post a Comment