Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL), Fimbo Butallah(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Mitumbwi kwa kanda ya Ziwa yanayodhaminiwa na Bia ya Balimi Extra Lager.Uzinduzi huo umefanyika Dar es Salaam leo.Kulia ni Mratibu wa mashindano hayo, Peter Zacharia.Picha kwa hisani ya Integrateg Comminication Limited.
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Balimi
Extra leo imetangaza rasmi kudhamini kwa mara nyingine tena mashindano ya mbio
za mitumbwi kwa wakazi wa kanda ya ziwa kwa mwaka huu 2013. Mashindano haya ya “kupiga makasia” yanafanyika kwa mwaka
wa kumi na nne mwaka huu na yamekuwa na hamasa na msisimko mkubwa kwa wakazi wa
maeneo hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam leo, Meneja Masoko wa kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Bwana Fimbo Butallah alisema kwamba lengo hasa la Bia ya Balimi Extra
kudhamini mashindano haya ni kufurahi pamoja na wakazi wa kanda ya ziwa hususani wale ambao ni wavuvi. Aliendelea kusema, “Mashindano haya yanaenzi na kulinda tamaduni zetu zisipotee, yanajumuisha watu mbalimbali kukutana, kufahamiana na kufurahi kwa pamoja na hii inasaidia sana kuimarisha amani na upendo baina yetu. Amani ni nguzo muhimu sana kwa Taifa letu”. Alisisitiza pia umuhimu wa michezo katika kujenga afya bora.
Bwana Fimbo alifafanua kwamba kwa mwaka huu mashindano ya mitumbwi yatahusisha miji mitano ya kanda ya ziwa. Yataanza rasmi mchakato wake Jumamosi hii tarehe 19 October katika mji wa Kigoma na kisha kuelekea mji wa Bukoba katika mkoa wa Kagera. Yataendelea mjini Mwanza, kisha katika kisiwa cha Ukerewe ambapo yatamalizikia katika mji wa Musoma. Washindi watakaopatikana katika miji hii watashindanishwa kwa pamoja ili kumpata mshindi wa kanda. Shindano la kumpata mshindi wa kanda linategemewa kufanyika jijini Mwanza mwanzoni mwa mwezi December. Tarehe za mashindano haya ni kama ifuatavyo;
1. Mji wa
Kigoma; Jumamosi tarehe 19
October Ufukwe wa Kibirizi.
2. Mji wa
Bukoba; Jumamosi tarehe 02
November Ufukwe wa Spice Beach.
3. Mji wa
Mwanza; Jumamosi tarehe 09
November Ufukwe wa Mwaloni.
4. Kisiwa
cha Ukerewe; Jumamosi 16 November Ufukwe Hoteli ya
Monarch.
5. Mji wa
Musoma; Jumamosi tarehe 23
November Ufukwe wa Bwalo la Polisi.
6. Mashindano
ya Kanda; Jumamosi tarehe 07 Dec Ufukwe Mwaloni, Mwanza.
Bwana Fimbo akizungumzia zawadi za mwaka huu alisema kwamba
katika ngazi ya mikoa na ngazi ya kanda Balimi Extra imetenga zaidi ya shilingi
milioni ishirini na nne kama zawadi za pesa taslimu kwa washindi. Mpangilio wa
zawadi ni kama inavyoonekana hapa chini;
ZAWADI
|
NGAZI YA MKOA
WANAUME
|
NGAZI YA MKOA
WANAWAKE
|
NGAZI YA KANDA
WANAUME
|
NGAZI YA KANDA
WANAWAKE
|
Mshindi wa Kwanza
|
900,000
|
700,000
|
2,700,000
|
2,300,000
|
Mshindi wa Pili
|
700,000
|
600,000
|
2,300,000
|
1,700,000
|
Mshindi wa Tatu
|
500,000
|
400,000
|
1,700,000
|
900,000
|
Mshindi wa Nne
|
400,000
|
300,000
|
900,000
|
700,000
|
Mshindi wa 5 - 10
|
6 @
250,000
|
6 @
200,000
|
6 @
400,000
|
6 @ 250,000
|
Bwana Fimbo alimaliza kwa kuwaomba wanachi wa kanda ya ziwa wajitokeze kwa wingi katika miji iliyotajwa ili kufurahi kwa pamoja katika matamasha haya. Alisisitiza wasisahau mila na tamaduni zao katika kipindi ambacho watu wengi hupenda kuiga tamaduni za kimagharibi. Alimaliza kwa kuwashukuru sana wanywaji wa bia ya Balimi Extra kwa kuchagua bia hii na kuomba waendelee kuitumia kwani ni kupitia mchango wao ndipo pia Balimi Extra Lager inaweza kuleta burudani kama hizi kwa ajili yao.
No comments:
Post a Comment