BUKOBA SPORTS

Friday, October 18, 2013

STOKE YAWASILISHA MALALAMIKO RASMI KUHUSU REFA ROGER EAST


Mtendaji mkuu wa Stoke City, Tony Scholes, amemwandikia Mkuu wa Marefa Mike Riley kulalamika kwao na kutoridhishwa na Refa Roger East aliechezesha pambano lao la Ligi Kuu England na Fulham walilofungwa Bao 1-0 huko Craven Cottage Mwezi uliopita.

Refa East, ambae Msimu huu ndio amepandishwa na kuingizwa Kundi la Marefa wanaochezesha Ligi Kuu, alimuudhi sana Meneja wa Stoke Mark Hughes kwenye Mechi hiyo na Fulham kwa kutoa maamuzi yenye utata ikiwa ni pamoja na kushindwa kumpa Kadi Nyekundu Mchezaji wa Fulham Pajtim Kasami kwa kumpiga Erik Pieters.

Mara baada ya Mechi hiyo Mtendaji Mkuu Tony Scholes alimpigia Simu Mike Riley ambae ndie Mkuu wa PGMOB, Professional Game Match Officials Board, Bodi ya Marefa.

Refa East Wikiendi hii hakupangiwa Mechi yeyote ya Ligi Kuu na Msimu huu amechezesha Mechi mbili tu za Ligi Kuu.
High marks: Referee Roger East
 Referee Roger East, Stoke’s 1-0 defeat by Fulham

No comments:

Post a Comment