BUKOBA SPORTS

Saturday, February 15, 2014

DAYNA NYANGE NA CINDY SANYU WA UGANDA WAFUNIKA NDANI YA UKUMBI WA JB BELMONTE HOTEL USIKU HUU VALENTINE DAY NDANI YA JIJI LA MWANZA.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Dayna Nyange akikamua vilivyo usiku huu wa Valentine Day katika Ukumbi wa JB Belmonte Hotel katika jiji la Rocky City (Mwanza) ambapo katika ukumbi huo huo alikuwepo na mkali  wa muziki Cindy Sanyu kutoka Nchini Uganda pamoja na wasanii wengine wa hapa jijini Mwanza.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Dayna Nyange akifanya mambo yake jukwaani usiku huu.
Dayna akiimba kwa hisia moja ya wimbo wake mbele ya mashabiki wake

Nivute kwako!!! ni wimbo wake msanii Dayna akiuimba vyema Jukwaani leo kwenye Ukumbi wa JB Belmonte Hotel katika jiji la Rocky City (Mwanza) leo Valentine Day.Dada Carol (kulia) akicheza pamoja na rafiki yake kumsindikiza msanii Dayna leo kwenye siku ya wapendano!
Dayna Nyange amekamua nyimbo zake kadhaa huku wadau wakimkubali zaidi katika ukumbi huu. Cha zaidi kwa Dayna hakuweza kuficha tabasamu lake huku akijua ni sikukuu ya Wapendanao hivyo amekamua kisawasawa!!!
Dayna akitoa tabasamu hapa!!! Mpaka Shabikia akamfata juu ya jukwaa!Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Dayna Nyange akicheza na Shabiki wake.Cindy Sanyu kutoka Nchini Uganda...akaingia kwa stage!! ukumbi ukawaka moto!!!Cindy Sanyu kutoka Nchini Uganda(katikati) akicheza kwa pamoja na wanamuziki wake kuwapa kile Wabongo walichomwitia katika ukumbi huu wa JB Belmonte Hotel. Majanga!! kazi ikakatika!Hakika katushika Cindy!!!

No comments:

Post a Comment