BUKOBA SPORTS

Saturday, November 22, 2014

ARSENAL 1 vs 2 MANCHESTER UNITED, WAYNE ROONEY AICHINJA GUNNERS EMIRATES!!


Kepteni wa Manchester united Wayne rooney akishangilia bao lao la kujifunga wenyewe Arsenal
WAKICHEZA Ugenini huko Emirates na Difensi ya kuungaunga iliyoongozwa na Chris Smalling akisaidiwa na Chipukizi Tyler Blackett na Paddy McNair na Mawinga wawili, Valencia na Ashley Young, Man United walifanikiwa kuwatwanga Arsenal Bao 2-1 na kuchupa hadi Nafasi ya 4 kwenye Msimamo wa Ligi Kuu.
Wakitumia Mfumo wa 3-4-1-2, Meneja wa Man United Louis van Gaal alifanikiwa kupata ushindi wake wa kwanza wa Ugenini kwenye Ligi baada ya kupata Mabao kupitia Mchezaji wa Arsenal Kieran Gibbs aliejifunga mwenyewe na Kepteni Wayne Rooney baada ya kaunta ataki.
Bao la Arsenal lilifungwa na Olivier Giroud alieingizwa kutoka Benchi akirejea Uwanjani baada ya kukaa Miezi Mitatu nje akiuuguza Mguu wake uliovunjika.
Licha ya kuanza na Difensi dhaifu, Man United pia walipata balaa katika Dakika ya 16 wakati Fulbeki Luke Shaw alipoumia enka na kubadilishwa na Winga Ashley Young.Wachezaji wa Man United wakipongezana kwa Ushindi waliupata pamoja na kuwa na kikosi kibovu sana. Wameitandika Arsenal Nyumbani kwake Emirates usiku huu bao 2-1Mchezo wa Ligi Kuu England.Rooney akishangilia bao lake baada ya kuifunga Arsenal bao la pili nakufanya 2-1 dhidi ya Wenyeji Arsenal katika Uwanja wa Emirates.Jack Wilshere of Arsenal reacts to an ankle injury Jack akiwa chini akijiuguza baada ya kuumiaArsenal's Jack Wilshere looks distraught after suffering an injury Kipindi cha pili dakika ya 56 Gibbs anajifunga bao na kuweka 1-0 dhidi ya timu yake Arsenal. man United wanaongoza kwa bao hilo huku Kipa wao Arsenal akibadilishwa baada ya kulazimika kutoka nje baada ya kuumia.Kipindi cha kwanza kimemalizika, hakuna aliyeziona nyavu za mwenzake katika kipindi cha kwanza. Timu ya Arsenal ikitawala zaidi kipindi hicho cha kwanza zaidi ya Man United. Kipigo hiki kwa Arsenal kimewaacha wakiwa Nafasi ya 8 na wana Pointi 17 kwa Mechi 12 wakiwa Pointi 15 nyuma ya Vinara Chelsea na huu ni msimamo wao wa chini kabisa katika Miaka 32.Mchezaji wa Zamani wa Man United kwa sasa wa Arsenal akiwa kwenye kujiuliza baada ya kuwakosa kosa bao United katika kipindi cha kwanza.Arsenal's Wojciech Szczesny watches Di Maria's shot fly past the postDi Maria akimwangaisha kipa wa Arsenal langoni mwake..Kipindi cha kwanza kimeanza...Arsenal wanafanya mashambulizi ya hapa na pale...
Olivier Giroud akipasha kabla ya Mtanange kuanza

No comments:

Post a Comment