Robert Lewandowski akiifungia bao Bayern Munich usiku huu dhidi ya Dortmund mpira uliomalizika kwa bao 1-0.
Wachezaji wa Bayern Munich wakishangilia Ushindi wa wa bao 1-0 usiku huu dhidi ya Dortmund
Robert Lewandowski Dakika ya 36 Kipindi cha kwanza aliifungia bao Bayern Munich.Mechi ya Bundesliga ambayo ina Jina la Ubatizo 'DER KLASSIKER' na kipigo hiki kikidhihirisha Msimu mbovu wa Borussia Dortmund wakibaki katikati ya Msimamo wa Ligi na Bayern kuelekea kutetea Taji lao.
Bao la ushindi la Bayern lilifungwa na Mchezaji wa zamani wa Dortmund Robert Lewandowski katika Dakika ya 36.
Ushindi huu umewapa Bayern uongozi wa Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Wolfsburg na Dortmund kubaki Nafasi ya 10.
Lewandowski hakushangilia baada ya kuipiga Timu yake ya Zamani Borussia Dortmund
Pep Guardiola akiongoza Benchi lake kushangilia..
Mfungaji wa Bao la pekee Lewandowski akichuana na Mchezaji wa Dortmund Kevin Kampl
Timu zikijipanga kabla ya Mtanange kuanza
No comments:
Post a Comment