YANGA YAFUNGWA 1-0 ZIMBABWE, YAFUZU KWA 5-2 KOMBE LA SHIRIKISHO, SASA KUIVAA BENFICA AU SAHEL!
Yanga imefanikiwa kuchanja mbuga katika michuano ya Kombe la Shirikisho kwa
jumla ya mabao 5-2 ikiwa ugenini nchini Zimbabwe.
Yanga wamefuzu licha ya kufungwa kwa bao 1-0 dhidi ya FC Platnum katika
mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Mandava ulio takribani Kilomita 200
kutoka mji wa Bulawayo.
Mechi hiyo kali na ya kuvutia, wenyeji walipania kufunga mabao manne ili
wafuzu lakini ilishindikana.
Kocha Hans van der Pluijm alilazimika kumtoa mapema kinda Said Juma
‘Makapu’ kutokana na kuonekana kuzidiwa na nafasi yake kumuingiza Kelvin
Yondani.
No comments:
Post a Comment