BUKOBA SPORTS

Friday, May 1, 2015

ROBIN VAN PERSIE APEWA ANGALIZO KWA MECHI 4 ZILIZOBAKI MSIMU HUU!! AKICHEMSHA KUPIGWA BEI!

Straika wa Man United robin Van Persie ameripotiwa kuwa anamechi nne tu zilizobaki msimu huu wa 2014/15 kuonesha Cheche zake ili kuokoa hatima yake ya kubaki Old Trafford la sivyo atapigwa chini mwishoni mwa msimu. Katika Mechi hizo 4 zilizobaki wenda akawa anapagwa katika kipindi cha kwanza. Katika Msimu huu Van Persie amecheza mechi 25 tu kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya enka lakini atakuwa na bahati ya kuanzishwa katika mechi hizo zilizobaki ili kuonesha kama kweli ataonesha mwitikio wa kuonesha ubavu wake kama anastahili kubaki kwa mashetani wekundu wa Old Trafford.

No comments:

Post a Comment