BUKOBA SPORTS

Saturday, May 2, 2015

WAYNE ROONEY FITI KUCHEZA LEO...MANCHESTER UNITED vs WEST BROM ALBION

Niko fiti kuwavaa West Brom Albion hii leo!
Huko Man United kulikuwa na wasiwasi kuwa Rooney hatacheza Mechi hii na WBA baada ya kuumizwa Gotini na kutolewa Dakika ya 88 walipofungwa 3-0 na Everton huko Goodison Park Jumapili iliyopita.
Lakini Jana akiongea na MUTV, Meneja wa Man United, Louis Van Gaal, amethibitisha kuwa Rooney yuko fiti na pia huenda Robin Van Persie akaanza baada ya Kati Wiki iliyopita kupachika Bao 2 kwenye Mechi ya Timu ya Vijana ya U-21.
Hata hivyo, Man United itawakosa Majeruhi Michael Carrick, Luke Shaw, Marcos Rojo, Jony Evans, Rafae na pia Phil Jones ambae ingawa hivi sasa yuko fiti lakini Mechi hii ni mapema mno kwake.
Van Gaal na msaidizi wake Giggs

No comments:

Post a Comment