BUKOBA SPORTS

Wednesday, September 30, 2015

MASHABIKI ARSENAL WATAKA MENEJA WAO APIGWE CHINI!! WANATAKA KUONA MABADILIKO, WATAKA NAFASI YA ARSENE WENGER ICHUKULIWE NA KLOPP!

WADAU wa Arsenal wamekuja juu na kudai Meneja wao Arsene Wenger sasa ameishiwa visingizio na umefika wakati atimuliwe na nafasi yake kuchukuliwa Jurgen Klopp.
Mmoja wa waliodai hivyo ni Piers Morgan ambae ni Mwandishi na Mwendesha Kipindi cha TV ambae alikasirishwa na Jana kutandikwa 3-2 na Olympiakos ya Ugiriki katika Mechi ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONS.
Hiki ni kipigo cha pili kwa Arsenal katika Kundi lao baada ya kuchapwa 2-1 na Dinamo Zagreb huko Croatia.
Piers Morgan alisema: “Ulikuwa ni uchezaji mbovu katika Mechi za Ulaya ambao sijapata kuuona katika muda wake wote Wenger akiwa Arsenal.”
Aliongeza: “Tulicheza ovyo dhidi ya Timu iliyofungwa mara zote 12 ikicheza England na kufungwa Mabao 37-3. Lakini Jana wametubamiza!” Morgan alilalamika: “Wenger Siku zote ana visingizio, mara Uwanja, mara Fedha, Bodi, Hali ya Hewa. Kila kitu ni visingizio lakini si yeye Wenger. Jana visingizio vimeisha. Ni yeye!”

Morgan amedai Kocha wa zamani wa Borussia Dortmund, Jurgen Klopp, ndio anafaa kumbadili Wenger.
Mechi zinazofuata kwa Arsenal kwenye Kundi F la UCL ni Mechi mbili mfululizo dhidi ya Bayern Munich ambao wameshinda Mechi zao zote 2 kwa kuzibamiza 3-0 Olympiakos huko Ugiriki na 5-0 Dinamo Zagreb huko Munich.

Hata katika msimu wa 05/06 ilikuwa wazi kwamba haikuwa rahisi kwa wao kutwaa uchampion na kwenye fainali wakiwa -0 uwanjani walifungwa na kikosi bora cha FC Barcelona. Rekodi za Arsenal barani ulaya zinaonesha namna Wenger alivyoshindwa kupambana na vigogo wengine barani humo. Pamoja na kusifiaa nchini England, rekodi zake za ulaya zinaonesha uwezo wake wa kuongoza na kuifundisha Gunners umeshindwa kumudu soka la ulaya.
Labda Wenger sasa ameifikisha Arsenal mahala ambapo inabidi ampe kijiti mwalimu mwingine, kufeli kushindwa kubeba taji lolote kubwa tangu kikosi chake kilipotwaa EPL bila kufungwa msimu wa 2003/04, Arsenal imekwama. Makombe mawili ya FA Cup bado hayakidhi haja bila uwepo wa taji la EPL au lolote la ulaya.
Arsenal, katika ardhi yanyumbani bado hawaonekani kama wataupata ubingwa hivi karibuni. Wenger ameunda kikosi chenye wachezaji wanaolipwa fedha nyingi sana – usajili wa fedha nyingi wa Alexis Sanchez na Mesut Ozili haujaimarisha timu ipasavyo. Timu inakosa wachezaji wanatakaoleta tija kwenye maeneo yenye udhaifu ambao kwa miaka zaidi ya mitano umeendelea kuwa tatizo kwenye timu. – hasa katika nafasi ya kiungo na ulinzi. Lakini udhaifu huu bado haujashughulikiwa inavyopaswa. Je Wenger bado ni mtu sahihi amwa kuipeleka Arsenal hatua nyingine au ndio ameshindwa kabisa kukubaliana na ushindani mpya wa Chelsea na Manchester City.

No comments:

Post a Comment