Shirika la Jambo Bukoba lisilo la Serikali linalojihusisha na maendeleo ya elimu na michezo Mkoani Kagera limefanya Bonanza la michezo kwa shule za Msingi kutoka Halmashauri zote za Wilaya na Manispaa ya Bukoba lilofanyika 29 Januari, 2016 katika viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Bukoba.
Bw. Clemence aliishukuru Serikali ya Mkoa wa Kagera kwa ushirikiano wanaoupata shirika la Jambo Bukoba katika kutekeleza majukumu yake aidha, aliwaomba wazazi kujitoa kushiriki katika kuwasaidia watoto wao katika upatikanaji wa uji na chakula shuleni ili watoto wacheze kwa afya njema na kushiriki kikamilifu katika masomo yao.
Mgeni rasmi katika Bonanza hilo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella ambaye katika hotuba yake alilipongeza sana Shirika la Jambo Bukoba kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Mkoa wa Kagera pia aliwashukuru wafadhili kutoka Ujerumani kwa kufadhili Jambo Bukoba Mkoani Kagera.
Aidha, Mhe Mongella aliliomba Shirika la Jambo Bukoba kushirikiana na Maafisa Elimu wa Wilaya na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi kuendesha vikao vya wadau katika kila shule ili kuwa na uelewa wa pamoja wa michezo katika Mkoa na kushirikisha shule nyingi zaidi kuliko ilivyo sasa shule moja kila Wilaya.
Bonanza hilo lilihusisha wananfunzi wanamichezo 240 kutoka katika shule za Msingi nane, wanafunzi 30 kila shule moja kutoka kila Halamashauri, wanafunzi hao wavulana 15 na wasichana 15 waliwakilisha kila Halmashauri wakiwa na walimu wawili wawili kutoka kila shule bingwa ngazi ya Wilaya.
Washindi waliopatikana katika mashindano ya bonanza la Mkoa wamezawadiwa shilingi 4,000,000/= kila shule na fedha hizo zitatumika katika kuimarisha miundombinu ya shule husika kama kujenga matundu ya vyoo, kukarabati madarasa na ofisi za walimu kwa kushirikiana na jamii ya eneo husika.
Shirika la Jamboa Bukoba mwanzilishi wake ni Bwana Clemence N. Mulokozi ambaye Baba yake ni mzaliwa wa Ishozi Wilayani Missenyi na mama yake ni Mjeurumani.
No comments:
Post a Comment