Habari za ndani zimedai Van Gaal alikutana na Woodward Jumapili na kisha kuruka kwenda kwao Netherlands kuhudhuria kile kilichoitwa Bethdei ya Binti wake wa Kike.
Lakini hali Klabuni hapo ni tete hasa kutokana na presha ya Mashabiki wa Klabu hiyo ambao Jumamosi walimzomea Van Gaal na kumtaka aondoke mara baada ya kufungwa 1-0 na Southampton Uwanjani Old Trafford.
Hicho kilikuwa kipigo chao cha 6 kwenye Ligi Kuu England Msimu huu na kimewatupa Nafasi ya 5 wakiwa Pointi 10 nyuma ya Vinara Leicester City na Pointi 5 nyuma ya Timu ya 4 ambayo ndiyo nafasi ya mwisho ya kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao.
Mbali ya kufungwa, Mashabiki wa Man United hawaridhishwi na staili ya uchezaji ya Van Gaal ambae msisitizo wake ni Difensi.
Huku Van Gaal akitarajiwa mwenyewe kubwaga manyaga badala ya kufukuzwa, zipo kila dalili Jose Mourinho huenda akachukua hatamu hasa baada ya kuvuja habari kuwa Mreno huyo aliandika Barua ya Kurasa 6 kwa Man United akielezea kufaa kwake kuongoza Timu hiyo.
No comments:
Post a Comment