Huko England, kuliibuka wimbi kubwa la kumlaumu Memphis kwa Pasi yake mbovu kwa Morgan Schneiderlin iliyotoa mwanya kwa Shambulizi la Chelsea katika Dakika za Majeruhi na kuzaa Bao la Diego Costa alipoifungia Chelsea Bao la kusawazisha.
Memphis, ambae ametimiza Miaka 22 Wiki hii, hajaanza Mechi yeyote ya Man United tangu Siku ya Boksing Dei ambapo Pasi yake mbovu kwa Kipa David de Gea ndio iliyozaa Bao la kwanza kwa Stoke City huko Britannia Stadium walipofungwa 2-0 na Stoke.
No comments:
Post a Comment