Inasemekana Rooney aliumia Wikiendi iliyopita Man United walipofungwa na Sunderland na sasa yupo hatarini kuzikosa Mechi 8 za Timu yake zikiwemo zile dhidi ya Arsenal, Man City na Tottenham.
Van Gaal alisema: "Anatufungia Bao nyingi na hivyo ni muhimu kwetu. Inabidi twende bila yeye."
Rooney, mwenye Miaka 30, hayupo huko Denmark na licha ya kuumia kwenye Mechi na Sunderland aliimaliza Mechi yote hiyo na Van Gaal amezungumzia hilo.
Pia, Timu ya Taifa ya England ambayo Mwezi Juni itacheza Fainali za Mataifa ya Ulaya, EURO 2016, huki France, itamkosa kwenye Mechi zao 2 za Kirafiki Mwezi Machi dhidi ya Germany na Netherlands.
No comments:
Post a Comment