Jana USA iliifunga Malaysia 2-1 na South Korea kutoka 0-0 na Wenyeji India na Matokeo hayo yalikamilisha Mechi za Kundi la Timu 5 na kuzipa USA na South Korea Nafasi 2 za juu za Kundi na hivyo kutinga Fainali watakapokutana wenyewe wakati Tanzania sasa imemaliza Nafasi ya 3 na itacheza na Malaysia, iliyomaliza Nafasi ya 4, kugombea Mshindi wa 3.
Juzi Tanzania ilimaliza Mechi za Kundi kwa kutoka Sare 2-2 na Malaysia.
Awali, Serengeti Boys ilitoka Sare 1-1 na USA, kuitandika India 3-1 na kutoka Sare 2-2 na South Korea.
India wametupwa nje baada ya kumaliza mkiani mwa Kundi.
MSIMAMO WA MWISHO WA KUNDI:
-Mashindano haya yanachezwa kuanzia Mei 15 hadi Mei 25 huko Tilak Maidan Stadium in Vasco, Goa Nchini India.
-Mashindano haya yana Hatua mbili za Kundi na za Mtoano.
-Timu 4 za juu za Kundi ambalo lina Timu 5 zitasonga kuingia Mtoano ambapo Timu mbili za juu zitacheza Fainali.
No comments:
Post a Comment