BUKOBA SPORTS

Monday, May 16, 2016

BILIC AOMBEA MAN UNITED WABEBE FA CUP ILI WEST HAM YAKE ICHEZE EUROPA MSIMU UJAO!

MENEJA wa West Ham United Slaven Bilic anaombea Manchester United itwae FA CUP ili wao wapate chansi ya kufuzu moja kwa moja kucheza UEFA EUROPA LIGI Msimu ujao.
Kwenye Mechi ya mwisho ya BPL, Ligi Kuu England, waliyocheza Jumapili West Ham walifungwa 2-1 Stoke City na kutoa mwanya kwa Southampton kushika Nafasi ya 5 na wao kukamata Nafasi ya 7 nje ya Nafasi za kucheza EUROPA LIGI.
Man United, ambao hawakucheza Mechi yao ya mwisho Jumapili dhidi ya Bournemouth baada ya Mechi hiyo kufutwa kwa sababu za kiusalama, wapo Nafasi ya 6 na hivyo watacheza EUROPA LIGI.

Lakini Man United wanaweza pia kucheza EUROPA LIGI ikiwa Jumamosi ijayo watanyakua FA CUP na hivyo nafasi nyingine ya kucheza EUROPA LIGI ikafunguka kwa Timu ya Nafasi ya 7 ambayo ni West Ham.

Endapo Man United watafungwa Fainali ya FA CUP na Crystal Palace basi West Ham wataikosa nafasi ya kucheza EUROPA LIGI kwani nafasi hizo zitaenda kwa Crystal Palace, kama Bingwa wa FA CUP, Timu ya 5 Southampton na Timu ya 6 Man United huku Man United wakiwa na nafasi ya kushika Nafasi ya 5 wakiifunga Bournemouth kwenye Mechi  yao ya mkononi itakayochezwa Jumanne Usiku na Southampton kukamata Nafasi ya 6.

Hali hii imemfanya Meneja wa West Ham United Slaven Bilic kusikitikia na kueleza: “Msimu wote tilikuwa maeneo ya kucheza Ulaya lakini tuliyumba Mechi 3 na 4 za mwisho. Sasa tunaombea Man United wabebe FA CUP ili sisi tucheze EUROPA LIGI!”

Msimu uliopita West Ham walifuzu kucheza EUROPA LIGI kwa Tiketi ya Uchezaji wa Haki lakini wakatolewa Raundi ya 3 ya Mchujo na Klabu ya Romania FC Astra Giurgiu.

No comments:

Post a Comment