Ripoti zimedai Mourinho, ambae atamrithi Louis van Gaal, alieondolewa Juzi, ameshakubali Urefu wa Mkataba na Maslahi yake binafsi lakini kikwazo kikubwa kinachochelewesha Dili kukamilika na Mkataba kusainiwa ni mgongano wa Umiliki wa Haki za Matangazo na Picha.
Pande hizo mbili zina Mikataba ya Kibiashara ambayo ni tofauti ambayo lazima yafikiwe makubaliano ili kusiwe na mgongano wa kimaslahi.
Lakini yapo maeneo kadhaa yenye mgongano na moja ni Mkataba wa Mourinho na Kampuni ya Magari ya Jaguar wakati Man United wana Mkataba wa Miaka 7 Kampuni ya Magari ya General Motors ambayo Gari yao aina ya Chevrolet nembo yake hubebwa kwenye Jezi za Man United.
No comments:
Post a Comment