Pogba aliondoka Man United Mwaka 2012 baada ya kuugomea Mkataba Mpya na kwenda Juventus na wakati huo aliekuwa Meneja wa Man United Sir Alex Ferguson kusema alitaka Kijana huyo abaki lakini Wakala wake, Mino Raiola, alikuwa ‘sumu’.
“Sikumwamini tangu Siku ya kwanza niliyokutana nae. Tulikuwa na Pogba kwa Mkataba wa Miaka Mitatu uliokuwa na Kipengele cha Nyongeza ya Mwaka Mmoja. Ghafla Raiola akaingia na Mkutano wetu wa kwanza ulikuwa balaa!”
“Yeye na mimi tulikuwa kama maji na mafuta. Na yeye akawarubuni Familia ya Kijana huyo na akasaini Juve!”
Tayari Raiola, ambae ni Wakala wa Mastaa Wawili Zlatan Ibrahimovic na Henrikh Mkhitaryan, ameshasuka Wachezaji hao kutua Man United.
Lakini huenda Dau la kumnunua Pogba, Karibu Euro Milioni 100, likawa kikwazo kwa Mchezaji alieondoka bure bila kulipwa Senti.
No comments:
Post a Comment