Mchezaji wa Arsenal Chuba Apkom alionyesha ukali wake kwa kupiga Bao 1 likiwa ni Bao lake la Nne katika Mechi Nne zilizopita.
Timu zote zilishusha Vikosi imara kwenye Mechi hii na City kutangulia kufunga kwa Bao la Sergio Aguero alieunganisha krosi ya Raheem Sterling katika Dakika ya 30.
Alex Iwobi akaisawazishia Arsena Dakika ya 50 na kisha Theo Walcott na Chuba Apkom kuipa Arsenal Bao 3-1 katika Dakika za 73 na 85.
Jana Arsenal walipata pigo jingine baada ya Sentahafu wao Gabriel kuumia alipogongana na Raheem Sterling na kulazimika kutolewa kwa Machela.
Kwenye Mechi hii, kila upande uliwatumia Wachezaji kadhaa kwa mara ya kwanza wakitokea Holidei ambapo kwa Arsenal walicheza Alexis Sanchez na Aaron Ramsey na kwa City walikuwepo Aguero na Nolito.
No comments:
Post a Comment