Lakini Meneja wa sasa wa Man United, Jose Mourinho, ametoboa anafurahia changamoto hizo na hataruhusu presha zimshinde.
Akiongea kuelekeaechi hii ya Leo, Mourinho ameeleza: “Sioni kama ni mzigo. Nahisi Historia kubwa ya Klabu hii ni kitu kizuri na siwazii mabaya. Tatizo ukipewa masharti ya kufuata!”
Man United wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa wameshinda Mechi 4 mfululizo katika Mashindano yote na kuzoa Pointi 9 kati ya 9 kwenye EPL.
Sunderland, walioanza Msimu vibaya, walijikongoja Mwezi Novemba wakishinda Mechi 2 kati ya 3 na Mwezi huu walishinda Mechi zao 2 za Nyumbani dhidi ya Leicester na Watford na kuleta matumaini mapya.
Wakati Man United wapo Nafasi ya 6, Pointi 3 nyuma ya Timu ya 5 Tottenham na 4 nyuma ya Arsenal ambao ni wa 4, Sunderland wapo Nafasi ya 18 wakiwemo kwenye zile 3 za Mkiani ambazo hushuka Daraja mwishoni mwa Msimu.
Msimu uliopita:
Man United waliichapa Sunderland 3-0 Uwanjani Old Trafford kwa Bao za Wayne Rooney, Memphis Depay na Juan Mata na kufungwa 2-1 huko Stadium of Light..
EPL, LIGI KUU ENGLAND
Ratiba:
Jumatatu Desemba 26
1530 Watford v Crystal Palace
1800 Arsenal v West Bromwich Albion
1800 Burnley v Middlesbrough
1800 Chelsea v Bournemouth
1800 Leicester City v Everton
1800 Manchester United v Sunderland
1800 Swansea City v West Ham United
2015 Hull City v Manchester City
No comments:
Post a Comment