BUKOBA SPORTS

Saturday, May 27, 2017

BEKI MKONGWE PATRICE EVRA AFURAHIA KUREJEA MANCHESTER UNITED

Patrice Evra has shopwed his delight at being called-up for Michael Carrick's testimonialInavyoonekana beki mkongwe Patrice Evra inaonekana bado ana mapenzi makubwa na Manchester United.
Beki huyo ambaye anaichezea Marseille ya Ufaransa, amekaribishwa kwenye kwenye Uwanja wa Old Trafford kwa ajili ya kucheza katika mechi ya hisani ya Michael Carrick itakayochezwa Juni 4, mwaka huu.
Evra aliichezea kuanzia mwaka 2006 hadi 2014 akiwa nai beki kipenzi cha mashabiki wengi wa timu hiyo hasa chini ya utawala wa Kocha Alex Ferguson.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Evra ameweka video fupi akiwa na jezi ya timu yake hiyo ya zamani akifurahia kurejea Manchester.
Evra sang along to Beyonce as he could not contain his glee at returning to Old TraffordKwa sasa umri wake ni miaka 36 ambapo inavyoonekana anaelekea kustaafu kucheza soka baada ya kupata mafanikio mengi ngazi ya klaby na timu ya taifa.

Alikuwa akiimba wimbo wa Beyonce huku akitamka kuwa “Nakuja nyumbani Fergie'.

Katika mchezo huo maalum, kuna wachezaji wengi waliowahi kutamba kikosini hapo watashiriki wakiwemo Park Ji-Sung, Mikael Silvestre, Owen Hargreaves, Louis Saha na Darren Fletcher.

Wengine ni Ryan Giggs, Paul Scholes na Gary Neville.

No comments:

Post a Comment