
Tripu hiyo itawafanya Everton watue Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kucheza Mechi 1 ya Kirafiki hapo Julai 13.
Mechi hiyo inatokana na mipango ya Kampuni kubwa ya Michezo ya Bahati Nasibu, SportPesa, ambayo imeingia ushirikiano na Everton hivi karibuni na pia kutua Tanzania kwa kishindo kwa kuzidhamini Klabu kadhaa kubwa zikiwemo Mabingwa Yanga, Simba na Singida United.

Hapo Julai 13, Everton, chini ya Meneja Ronald Koeman, watacheza na Bingwa wa Mashindano Mapya ya SportPesa SUPER CUP ambayo yatashirikisha Klabu 4 za Kenya na 4 za Tanzania.
SportPesa, Kampuni iliyoanzishwa Mwaka 2014, imeingia kwa kishindo kwenye Michezo hasusan Soka, ikitangaza Biashara yao ya Bahati Nasibu hasa zinazochezwa Mitandaoni.
No comments:
Post a Comment