BUKOBA SPORTS

Wednesday, March 28, 2012

CHELSEA NA REAL MADRID NDANI YA NUSU FAINALI UEFA.

SOLOMON KALOU AICHOMA BENFICA


                                               Salomon Kalou aifungia Chelsea bao

Bao la Salomon Kalou iliisaidia timu ya Chelsea kuingiza mguu mmoja katika hatua ya nusu fainali ya kombe la mabinwa bara ulaya baada ya kuwachapa wenyeji wao Benfica ya Ureno.

Fernando Torres (katikati) wa Chelsea na Jardel (kulia) wa Benfica usiku wa jana kwenye Uwanja Estadio da Luz, Lisbon.
Mwamba huyo wa Ivory Coast alifunga bao hilo la pekee katika daikia ya 75 baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Fernando Torres ambaye nae katika mechi hii alikuwa katika hali nzuri.
                               
Hapo awali Kalou alipoteza nafasi kadhaa za kufungo mabao.
Kauli ya Drogba iliyodaiwa awali na kocha wa Benfica kuwa ilikuwa ya kejeli kwa timu yake na kutaka kauli hiyo ijibiwe kwa kipigo kwa Chelsea, goli la Kalou lilionekana kuipa nguvu zaidi kauli hiyo na huenda hata kocha mwenyewe Jorge Jesus ameumia zaidi kwani dhamirra yake ya kuwaadhibu Chelsea haikutokea.
Kocha wa Chelsea Roberto Di Matteo katika kuhakikisha anapata ushindi, aliwatumia wachezaji wake wenye uzoefu mkubwa na uchezaji wa timu za Ureno.

          Kalou, Mata na Torres wakishangilia baada ya timu yao kufunga goli, chelsea walishinda 1.0

Wachezaji wa zamani wa Benfica kama vile kina David Luiz, Ramires, Raul Meireles na Paulo Ferreira ndio waliopewa kibarua cha kuihangaisha timu yao ya zamani.

No comments:

Post a Comment