BUKOBA SPORTS

Monday, March 26, 2012

MH. PINDA APOKEA KOMBE LA UEFA LEO HII DAR NA PIA KUAGANA NA BW. OLUSEYI                                          


Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiwapungua watu waliofika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kushuhudia wakati alipokabidhiwa kombe la UEFA jijini Dar es salaam Machi 26, 2012





 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda kwa pamoja na Meneja Mkuu wa Bia ya Heinken Afrika Mashariki Bw.KoenMorshiu's wakifunua kitambaa, kuonyesha kombe la Ulaya wakati Kampuni ya bia ya Heinken ambao ndiyo wadhamini wa kombe la Ulaya (UEFA) walipomkabidhi kombe hilo waziri mkuu leo ofisini kwake, Kampuni ya Henken pamoja na Shirikisho la mpira wa miguu la ulaya (UEFA) liko katika ziara ya kulitembeza kombe hilo katika nchi za Afrika na Amerika ya Kusini nchini Mexico na Asia nchini China na Tanzania na Kenya.


Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipiga picha na Kombe hilo pamoja na mawaziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, kulia ni Naibu Waziri wa wizara hiyo Dk Fenella Mukangara, wa pili kutoka kushoto ni Dk Emmanuel Nchini Waziri wa wizara hiyo na Makamu wa kwanza wa shirikisho la mpira miguu nchini Tanzania (TFF) Athuman Nyamlani.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu. 







  
Hapa ni waziri mkuu akipokea kinyago kwa mwakilishi wa shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi. Bwana Oluseyi Bajulaye ambaye alikwenda kuaga leo katika ofisi ya waziri mkuu.


KOMBE LA UEFA.
Kombe la Mabingi wa wa Ligi ya Ulaya (UEFA) limetua nchini na leo Amekabidhiwa rasmi  Waziri Mkuu wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda.
 
Meneja Uhamasishaji wa Heineken, Hans Erik Tuijt, alisema mwishoni mwa wiki kwamba ziara ya kombe hilo katika nchi mbalimbali duniani inalenga kuwaweka mashabiki wa soka karibu na mwaka huu ni nafasi ya Watanzania kuliona.
Tuijt alisema kwamba hii ni mara ya sita kombe hilo kutembezwa kuanzia msimu wa mwaka 2005/06 ambapo wanatumia nafasi hiyo kuzungumza na wateja wao kupitia mchezo wa mpira ambao unapenda na mashabiki wengi duniani.
Alisema kuwa kombe hilo hapa nchini limekuja likitokea jijini Nairobi nchini Kenya ikiwa ni nchi mbili pekee zilizoteuliwa kutembelewa barani Afrika.


Aliongeza kuwa wakati mashindano ya kombe hilo yakielekea fainali, wenyeji wa kombe hilo wamesema kwamba wataendelea kushikamana na mashabiki kwa kuonyesha uzoefu huo wa kihistoria. 


No comments:

Post a Comment