Antolin Alcaraz (wa pili kushoto) akishangilia Wigan kupanda daraja (Premier League survival)
Bao la Dakika ya 87 la Antolin Alcaraz kwenye Mechi ya Ligi kuu England iliyochezwa jana Ewood Park limewapa Wigan ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Blackburn Rovers na kuhakikisha usalama wao kubaki Ligi Kuu England na pia kuwaporomosha Daraja Blackburn Rovers ambao wanaungana na Wolves kucheza Ligi ya Npower Championship Msimu ujao.
Hadi sasa bado kujulikana Timu ya 3 itakayoungana na Blackburn na Wolves kushuka Daraja lakini itakuwa ni kati ya Bolton, QPR au hata Aston Villa ingawa hawa wanalindwa na ubora wa tofauti ya magoli.
Kwa muda mrefu Mashabiki wa Blackburn wameonekana wakilalamika kumpinga Meneja Steve Kean pamoja na Wamiliki wa Klabu hiyo, Kampuni ya kuuza Kuku ya Kihindi Venky’s, na jana mmoja wa Mashabiki hao alimtoa Kuku alievalishwa Jezi ya Blackburn na Kuku huyo akatinga Uwanjani kwenye Dakika ya 8 na kusababisha pambano lisimame hadi pale Kipa wa Wigan, Al Habsi, alipomnyakua Kuku huyo na kuwapa Walinzi.
Kabla ya Mechi za mwisho za Ligi Kuu England kwa Msimu huu kuchezwa Jumapili ijayo Mei 13, Jana timu ya Wigan ilifanikiwa Usiku kuifunga Blackburn goli 1-0 kwa kile kiporo cha Mechi yao, Blackburn Rovers walikuwa kwao kupigana na Wigan Athletic kwenye Mechi ambayo ilikuwa ngumu sana na muhimu kwa vile kila Timu ilikuwa inawinda ushindi ili kujinusuru balaa la kushushwa Daraja. mfungaji wa bao hilo akiwa ni Antolin Alcaraz goli la kichwa la dk ya 87.
Steve Kean baada ya timu yake kufungwa alionekana kuchoka na huku kelele za mashabiki zikizidi
Kituko, mechi ikiendelea alionekana kuku wa Blackburn uwanjani na mechi kusimamishwa kwa muda mpaka alipokamatwa na kipa Ali Al Habsi kwa kushirikiana na Yakubu, kuku huyo kuchukuliwa na polisi nje wa uwanja.
VIKOSI
Blackburn: Robinson, Orr, Dann, Givet, Martin Olsson, Hoilett, Dunn, Lowe, Pedersen, Modeste, Yakubu
Akiba: Kean, Formica, Petrovic, Nzonzi, Rochina, Marcus Olsson, Goodwillie.
Wigan: Al Habsi, Alcaraz, Caldwell, Figueroa, Boyce, McArthur, McCarthy, Beausejour, Moses, Di Santo, Maloney
Akiba: Pollitt, Crusat, Ben Watson, Gomez, Sammon, Rodallega, Diame.
Refa: Mark Clattenburg Yakubu na Ali Al Habsi wakiwa kwenye kamata kamata ya kuku uwanjani
Al Habsi akafanikiwa kumkamata kuku huyo kwenye neti za goli
Adui wa Rovers iliyohitaji ushindi tu kwenye mechi ya jana ili kubaki Ligi Kuu alikuwa ni Antolin Alcaraz aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 87 Uwanja wa Ewood Park.
Barclays Premier League
Barclays Premier League
Pos | Team | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Man City | 37 | 27 | 5 | 5 | 90 | 27 | 63 | 86 |
2 | Man Utd | 37 | 27 | 5 | 5 | 88 | 33 | 55 | 86 |
3 | Arsenal | 37 | 20 | 7 | 10 | 71 | 47 | 24 | 67 |
4 | Tottenham | 37 | 19 | 9 | 9 | 64 | 41 | 23 | 66 |
5 | Newcastle | 37 | 19 | 8 | 10 | 55 | 48 | 7 | 65 |
6 | Chelsea | 36 | 17 | 10 | 9 | 62 | 41 | 21 | 61 |
7 | Everton | 37 | 14 | 11 | 12 | 47 | 39 | 8 | 53 |
8 | Fulham | 37 | 14 | 10 | 13 | 48 | 49 | -1 | 52 |
9 | Liverpool | 36 | 13 | 10 | 13 | 43 | 38 | 5 | 49 |
10 | West Brom | 37 | 13 | 8 | 16 | 43 | 49 | -6 | 47 |
11 | Sunderland | 37 | 11 | 12 | 14 | 45 | 45 | 0 | 45 |
12 | Swansea | 37 | 11 | 11 | 15 | 43 | 51 | -8 | 44 |
13 | Norwich | 37 | 11 | 11 | 15 | 50 | 66 | -16 | 44 |
14 | Stoke | 37 | 11 | 11 | 15 | 34 | 51 | -17 | 44 |
15 | Wigan | 37 | 10 | 10 | 17 | 39 | 60 | -21 | 40 |
16 | Aston Villa | 37 | 7 | 17 | 13 | 37 | 51 | -14 | 38 |
17 | QPR | 37 | 10 | 7 | 20 | 41 | 63 | -22 | 37 |
18 | Bolton | 37 | 10 | 5 | 22 | 44 | 75 | -31 | 35 |
19 | Blackburn | 37 | 8 | 7 | 22 | 47 | 76 | -29 | 31 |
20 | Wolverhampton | 37 | 5 | 10 | 22 | 38 | 79 | -41 | 25 |
No comments:
Post a Comment