BUKOBA SPORTS

Friday, May 4, 2012

RAMSEY NOUAH: NATAKA KUFANYA FILAMU ZA VIWANGO NA HESHIMA TU KWA SASA

RAMSEY NOUAH ametamka hadharani kwamba hakuna jinsi utakavyoitaja fani ya filamu Nigeria uache kumgusa, lakini anafikiria kukaa pembeni kabla hajachuja
Msanii huyo alisema; "Najua mashabiki wangu watataka kuniona siku zote kwenye runinga, lakini kama ilivyo kawaida, lazima ung'atuke ukiwa bado unapendwa.
Najua nimefanya mambo makubwa sana kwenye hii tasnia, hakuna jinsi utakavyotaja jina Nollywood uache kunitaja."
"Nitakuwa naigiza hapa na pale lakini kidogo sana, nitakuwa nafanya sana mambo ya uongozaji, kuna kipindi kirefu sasa sijaonekana kwenye runinga kwa sababu sitaki kufanya kazi ambazo hazina viwango.
RAMSEY NOAH (KUSHOTO) AKIWA NA MAREHEMU KANUMBA (KULIA)
"Sitaki kufanya kazi ilimradi, nataka kuhusishwa na filamu zenye viwango na heshima kwenye hii fani."

No comments:

Post a Comment