BUKOBA SPORTS

Friday, June 15, 2012

DOGO JANJA AKIWA NJIANI KURUDI ARUSHA NGARENAROO

Picha juu na chini ni Dogo Janja akifanya vitu vyake
Nyota wa muziki wa kizazi kipya kutoka ‘kruu’ ya Tip Top Connection yenye maskani yake pande za Manzese jijini Dar es Salaam Abdul Abubakar Chende ‘Dogo Janja’ ametupiwa virago ndani ya kundi hilo.

Akizumngumza na Vijimambo mapema leo kiongozi wa kundi hilo Hamad Ally ‘Madii’ amesema kuwa Dogo Janja ameshindwa kuendana na makubaliano halisi yaliyokuwepo baina yake na uongozi wa kundi hilo ikiwemo kuhudhuria shuleni kama alivyokuwa akitakiwa kufanya kila siku badala yake amekuwa akiendekeza starehe na wakati mwingine kufanya mambo ambayo kwa namna moja ama nyingine yalikuwa yanalichafua kundi hilo.

No comments:

Post a Comment