BUKOBA SPORTS

Tuesday, June 19, 2012

EURO 2012: ENGLAND WAFURAHIA MCHEZO WAO NA UKRAINE KWA MSHAMBULIAJI WAO ROONEY KUCHEZA!

NAHODHA wa timu ya taifa ya England, Steven Gerrard amesema ana matumaini kurudi uwanjani kwa mshambuliaji Wayne Rooney kutaisaidia sana England hasa katika mechi ya leo watakapokuwa wakicheza na Ukraine.Final countdown: England need a point to ensure safe passage in to the quarter-finals
Rooney alikosa mechi mbili za hatua ya makundi kwa sababu alikuwa akitumikia adhabu ya kadi nyekundu aliyokuwa ameipata katika mechi ya kuwania kufuzu kucheza mashindano hayo ya Euro 2012.
Wide open spaces: England will face the co-hosts at the Donbass Arena
Mashambuliaji huyo mashuhuri wa England alipata kadi hiyo nyekundu katika mechi dhidi ya Montenegro, lakini amemaliza adhabu yake na anatarajiwa kuikabili Ukraine huko mjini Donetsk.
Wide open spaces: England will face the co-hosts at the Donbass Arena
"Wayne kurudi uwanjani ni faida kubwa kwetu na atatuongezea nguvu katika safu ya ushambuliaji, nilisema kabla hatujaanza kushiriki mashindano haya kwamba jambo la msingi ni kuhakikisha tunafanya vizuri katika mechi mbili za mwanzo kabla Wayne hajarudi uwanjani, na kweli tumepata pointi nne ambazo siyo mbaya,"alisema Gerrard.No guarantees: Ukraine are battling for a place in the quarter-finals
"Tunaamini Wayne atatusaidia na ataongeza morali wa wachezaji, mashabiki watakuwa na nguvu zaidi ya kutushangilia kila mtu England atakuwa na furaha kuona mshambuliaji nyota wa England, Wayne atakapokuwa amerudi uwanjani,"alisema Gerrard.
Head-to-head: Two veterans of the game will do battle on Tuesday night in Donetsk
Alisema,"Wayne alikuwa hafurahii hata kidogo kukosa mechi zetu mbili tulizocheza, Wayne anapenda soka, anatamani awepo uwanjani."
Akimzungumzia Wayne Rooney kocha wa England, Roy Hodgson alisema,"Wayne ni mchezaji mwenye ubora wa hali ya juu, naweza kusema ni mchezaji soka wa kidunia."

Alisema,"unakuwa na bahati ukiwa kocha wa timu ya taifa halafu una wachezaji kama Wayne katika kikosi chako, nilikuwa sifurahii kumkosa Wayne, lakini hivi sasa amerudi naamini na matokeo ya mechi zetu zijazo yatakuwa tofauti."

"Mimi sina wasiwasi kuhusu Wayne ila naamini ataleta mabadiliko makubwa katikia kikosi changu na Wayne hakumbushwi wajibu wake kwa sababu anajua anachotakiwa kufanya,"alisema Hodgson.
Hodgson alisema,"unajua katika kundi letu kila timu ina wachezaji wenye ubora wa kidunia ila sisi tulikuwa tuna mkosa mmoja, ninasema hivyo kwa sababu Sweden inaye Zlatan Ibrahimovic , Ukraine inaye Andriy Shevchenko,  Ufaransa inao Franck Ribery na Samir Nasri, sisi tulikuwa na Gerrard tu, lakini hivi sasa tutakuwa na Wayne pia.

No comments:

Post a Comment