BUKOBA SPORTS

Thursday, June 21, 2012

EURO 2012: WA KUANZA ROBO FAINALI LEO CZECH REPUBLIC VS PORTUGAL!

Leo Alhamisi Juni 21 huko Warsaw, Poland Robo Fainali ya kwanza ya EURO 2012 itachezwa kati ya Czech Republic na Portugal.
Wakati Portugal hawana majeruhi baada ya kupona Bruno Alves na Raul Meireles, Czech Republic wana wasiwasi na Nahodha wao Tomas Rosicky ambaye bado ana maumivu mguuni na upo uwezekano mkubwa asicheze Mechi hii.
Bila shaka, kwa Portugal, tegemezi kubwa ni Ronaldo ambae aliwika sana kwenye Mechi yao ya mwisho ya Kundi lao alipofunga bao zote mbili walipoipiga Holland bao 2-1.
Portugal na Czech Republic zimeshawahi kucheza mara 12 na kila Timu kushinda mara 4.

RATIBA
ROBO FAINALI
[Mechi zote Saa 3 Dak 45 Usiku]
Alhamisi Juni 21
RF1: Warsaw, Poland: Czech Republic v Portugal
Ijumaa Juni 22
RF2: Gdansk, Poland: Germany v Greece
Jumamosi Juni 23
RF3: Donetsk, Ukraine: Spain v France
Jumapili Juni 24
RF4: Kiev, Ukraine: England v Italy
NUSU FAINALI
[Mechi zote Saa 3 Dak 45 Usiku]
Jumatano Juni 27
NF1: Donetsk, Ukraine: Czech Republic/Portugal v Spain/France
Alhamisi Juni 28
NF2: Warsaw, Poland: Germany/Greece v England/Italy
FAINALI
Jumapili Julai 1
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Kiev, Ukraine: NF1 v NF2

No comments:

Post a Comment