BUKOBA SPORTS

Sunday, July 29, 2012

ARSENAL WATOSHANA NGUVU KWA SARE YA GOLI 2-2 HONG KONG NA TIMU YA KITCHEE

Katika Mechi ya leo dhidi ya Kitchee, Arsenal mara mbili walitoka nyuma na kusawazisha na kumaliza Mechi yao ya mwisho Barani Asia kwa droo ya 2-2 Ziara ambayo walianza kwa ushindi huko Malaysia na kufuatia na kipigo toka kwa Mabingwa wa England Manchester City Mjini Beijing, China.
KitChee walitangulia kupata bao baada ya kosa la Ignasi Miquel na Yago akafunga lakini mchezo mzuri wa Abou Diaby ulimfungulia Theo Walcott alienda kufunga bao la kusawazisha.
Lakini Dakika chache baadae Arsenal walijikuta wakipigwa bao la pili baada ya Kipa Wojciech Szczesny kuutema mpira wa Cheng Siu Waii na Dani Cancela akafunga.
Kipindi cha Pili Arsenal wakasawazisha tena kupitia Eisfeld baada ya kazi njema ya Gervinho.
Mechi inayofuata ya Arsenal ya kujipima nguvu ni Agosti 12 dhidi ya Cologne ya Ujerumani na Mechi hii itampa nafasi Mchezaji mpya Lukas Podolski kucheza dhidi ya Klabu yake ya zamani.

KIKOSI CHA ARSENAL KILICHOANZA
Szczesny, Eastmond, Miquel, Djourou, Gibbs, Diaby, Coquelin, Oxlade-Chamberlan, Walcott, Miyaichi, Chamakh

Respect: Theo Walcott scored Arsenal's first equaliser, slotting home confidently
Theo Walcott akitupia kusawazisha mara baada ya kupata pasi safi ya Abou Diaby

Respect: Theo Walcott scored Arsenal's first equaliser, slotting home confidentlywalcott akiwa kwenye atua ya kufurahia bao baada ya kutupia
 
kijana mdogo Ryo Miyaichiwa akichuana kuupata mpira

Development: Abou Diaby continued his pre-season, perhaps the most important of his career
Head boy: Young centre-back Kyle Bartley was also given a chance to impress once again

JACK WILSHERE KURUDI UWANJANI MWEZI OKTOBA

Arsene Wenger amesema kuwa Mchezaji wake Jack Wilshere hawezi kurudi Uwanjani hadi Mwezi Oktoba.
Wilshere, Miaka 20, aliukosa Msimu wote wa 2011/12 akisumbuliwa na enka na Mwezi Mei akafanyiwa operesheni ya goti.
Wenger amethibitisha kuwa wanategemea kumpata tena Kiungo huyo hodari Mwezi Oktoba na inategemewa kuwa katika Siku chache zijazo ataanza mazoezi mepesi.

kwa msaada wa sokainbongo

No comments:

Post a Comment