BUKOBA SPORTS

Monday, July 30, 2012

KOCHA WA ARSENAL- ARSENE WENGER AKIRI KUWA HANA DIFENSI NZURI KWENYE TIMU AKE!

Mara baada ya kumaliza Ziara yao Barani Asia, kufuatia sare ya 2-2 na KitChee ya Hong Kong, Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekiri Difensi yake, ambayo ilibandikwa bao 5 katika Mechi 3 za Ziara hiyo, ni ‘nyanya’ na inabidi iimarike kwa ajili ya Msimu mpya wa Ligi Kuu England unaoanza Agosti 18.
Akionyesha kusikitishwa kwake huku akikiri Wachezaji kadhaa waliokuwemo kwenye Ziara hiyo hawakuwa fiti, Wenger alitamka: “Difensi yetu inaonekana bado dhaifu hasa kwenye Kipindi cha Kwanza na KitChee. Tuna kazi kubwa.” 

Katika Mechi tatu ilizocheza huko Asia, Difensi ya Arsenal iliruhusu bao 5 pale ilipoifunga Kombaini ya Malaysia bao 2-1, ilipofungwa 2-0 na Manchester City na kutoka sare 2-2 na KitChee.
Wenger aliongeza: “Tuliruhusu kila Mtu acheze lakini baadhi hawajafikia kiwango cha Ligi Kuu. Wanajifunza. Kama hujifunzi kwenye Mechi hizi za kujipima huwezi tena, nimewapa nafasi wajue nini kinahitajika kwenye kiwango hiki cha juu. Niliwachezesha Madifenda wote lakini nyumbani wapo Madifenda wazoefu tuliowaacha, yupo Sagna, yupo Koscielny, yupo Mertesacker, wote hawa wazoefu wakubwa!”
Hi-res-143895497_crop_exact
Kwenye Mechi hiyo na Kitchee Difensi ya Mtu 4 ilianza na Kieran Gibbs, Johan Djourou, Ignasi Miquel na Craig Eastmond.
SORCE: SOKAINBONGO

No comments:

Post a Comment