Daktari wa Yanga, Juma Sufian, akimtibu Said Bahanuz huku akisaidiwa na watoa msaada wa Msalaba Mwekundu.
Mabingwa wa Kombe la Kagame, Yanga ya Dar es Salaam juzi iliichapa timu ya The Express ya Uganda mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa juzi Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Timu hiyo ndiyo mabingwa wa Ligi Kuu ya nchini humo. Katika mechi hiyo Yanga ilichezesha wachezaji wake wapya.
No comments:
Post a Comment